Bakita haijatoa ufafanuzi wa maneno haya

March 15, 2023 2:21 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni maneno yaliyojipatia umaarufu hivi karibuni.
  • Maneno ya ‘famasiala nini’, ‘famchezo nini’ pamoja na ‘fautani nini’.
  • Wazushi waghushi barua ya Bakita kukataza maneno hayo.

Dar es Salaam. Baraza la Kiswahili Tanzania (Bakita) limesema halijatoa ufafanuzi wowote kuhusu matumizi ya baadhi ya maneno yaliyojipatia umaarufu hivi karibuni ikiwemo ‘famasiala’.

Ipo taarifa inayosambaa katika mitandao ya kijamii ikiwemo Twitter inayodaiwa kuwa ya Bakita inaeleza kuwa baraza hilo limepiga matumizi ya maneno ya ‘famasiala nini’ , ‘famchezo nini’ pamoja na ‘fautani nini’

Bakita kupitia ukurasa wao wa Twitter leo Machi 15, 2023 imesema taarifa hiyo siyo ya kweli.


Soma zaidi


Hii si mara ya kwanza kwa baadhi watu kughushi taarifa na mabango mbalimbali yanayotolewa na baraza hilo jambo ambalo ni kinyume na sheria.

Huenda barua hiyo ya kughushi imetengenezwa kwa lengo la utani kutokana na maneno kama ‘famasiala nini’ , ‘famchezo nini’ pamoja na ‘fautani nini’ kujipatia umaarufu mkubwa mitaani na kwenye mitandao ya kijamii licha ya kutokuwa sanifu.

Kwa mujibu wa Sheria namba 27 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Baraza la Kiswahili pekee ndilo lenye mamlaka ya kutoa ufafanuzi wa matumizi sahihi ya maneno ya Kiswahili pamoja na kufanya usanifishaji wa meneno mapya.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

Nukta TV