Bakita haijatoa ufafanuzi wa maneno haya
- Ni maneno yaliyojipatia umaarufu hivi karibuni.
- Maneno ya ‘famasiala nini’, ‘famchezo nini’ pamoja na ‘fautani nini’.
- Wazushi waghushi barua ya Bakita kukataza maneno hayo.
Dar es Salaam. Baraza la Kiswahili Tanzania (Bakita) limesema halijatoa ufafanuzi wowote kuhusu matumizi ya baadhi ya maneno yaliyojipatia umaarufu hivi karibuni ikiwemo ‘famasiala’.
Ipo taarifa inayosambaa katika mitandao ya kijamii ikiwemo Twitter inayodaiwa kuwa ya Bakita inaeleza kuwa baraza hilo limepiga matumizi ya maneno ya ‘famasiala nini’ , ‘famchezo nini’ pamoja na ‘fautani nini’
Bakita kupitia ukurasa wao wa Twitter leo Machi 15, 2023 imesema taarifa hiyo siyo ya kweli.
— Baraza la Kiswahili la Taifa – BAKITA (@bakita_tz) March 15, 2023
Soma zaidi
-
Lhrc yajitosa mchakato usioridhisha upatikanaji wa haki mahakamani
-
Elimu ya bima itakavyopunguza ajali za barabarani
Hii si mara ya kwanza kwa baadhi watu kughushi taarifa na mabango mbalimbali yanayotolewa na baraza hilo jambo ambalo ni kinyume na sheria.
Huenda barua hiyo ya kughushi imetengenezwa kwa lengo la utani kutokana na maneno kama ‘famasiala nini’ , ‘famchezo nini’ pamoja na ‘fautani nini’ kujipatia umaarufu mkubwa mitaani na kwenye mitandao ya kijamii licha ya kutokuwa sanifu.
Kwa mujibu wa Sheria namba 27 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Baraza la Kiswahili pekee ndilo lenye mamlaka ya kutoa ufafanuzi wa matumizi sahihi ya maneno ya Kiswahili pamoja na kufanya usanifishaji wa meneno mapya.
Latest