Bajeti 2022-23 kutoa unafuu wa maisha, kufufua uchumi Tanzania

June 14, 2022 3:23 pm · David
Share
Tweet
Copy Link
  • Itasaidia kuleta unafuu kwa wananchi
  • Uchumi kufufuliwa baada ya kuathiriwa na Uviko-19 na vita ya Urusi na Ukraine
  • Mapambano ya vitendo vya rushwa kutiliwa mkazo.

Dar es Salaam. Serikali ya Tanzania imesema mapendekezo yaliyopo kwenye bajeti ya mwaka wa fedha wa 2022/23 yamelenga kutoa nafuu ya maisha kwa wananchi pamoja na kufufua uchumi baada ya kuathiriwa na Uviko-19 na madhara ya vita ya Urusi na Ukraine. 

Katika hotuba yake ya makadirio ya mapato na matumizi ya mwaka 2022/23 Waziri wa Fedha na Mipango Dk Mwigulu Nchemba amesema Uviko-19 na vita inayoendelea Ulaya Mashariki imeathiri mwenendo wa uchumi na sasa Serikali inaangazia namna ya kuwapatia Watanzania ahueni. 

“Nchi ya Urusi ni ya pili katika uzalishaji wa gesi asilia na bidhaa za mafuta ya petroli duniani. Kadhalika, nchi ya Ukraine ni miongoni mwa nchi zinazozalisha mafuta ya alizeti kwa wingi duniani. Kufuatia madhara haya ya vita, ni dhahiri kuwa uchumi na gharama za maisha duniani hazitabaki zilivyokuwa awali,” Dk Nchemba amesema.

Dk Mwigulu amesema bungeni jijini Dodoma leo (Juni 14, 2022) kuwa bajeti hiyo itatilia mkazo sera za mapato, sera za matumizi, kujali ufanisi (Value for Money), mapambano ya vitendo vya rushwa na kuwekeza kwenye sekta za uzalishaji ili kutengeneza ajira kwa vijana. 

Dk Nchemba ameongeza kuwa kwa mujibu wa Shirika la Chakula Duniani, nchi za Urusi na Ukraine ni kati ya nchi zenye uzalishaji na uuzaji mkubwa wa mazao mbalimbali ikiwemo ngano, mafuta ya kula na shayiri.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
6 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
6 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

Nukta TV