Asilimia 0.2 waliojiunga JKT wakutwa na VVU

February 5, 2023 6:51 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link

  • Vijana 147 kati ya 67,299 waliojiunga na jeshi hilo kati ya 2019 na 2021 walikutwa na VVU.
  • Kamati ya Bunge yashauri elimu iongezwe miongoni mwa vijana.

Dar es Salaam. Asilimia 0.2 ya vijana waliojiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) katika kipindi cha miaka mitatu wamekutwa na maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU).

Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi ya Februari 2022 hadi Februari 2023 iliyowasilishwa bungeni jijini Dodoma Februari 3 mwaka huu imeeleza kuwa vijana 147 kati ya 67,299 waliojiunga na jeshi hilo miaka mitatu walikutwa na VVU.

Vijana hao ni wale waliomaliza kidato cha sita ambao walijiunga na JKT kati ya mwaka 2019 na 2021. 

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mwaka 2019, vijana waliojiunga JKT walikuwa 20,413 ambapo kati yao 60 walikutwa na maambukizi wakati 2020 walijiunga vijana 21,383 na maambukizi yalikuwa kwa vijana 45.

Mwaka 2021 walijiunga vijana 25,503 na 42 kati yao ndiyo walikutwa na VVU.

Kamati hiyo katika taarifa yake imependekeza mkakati wa kupima na kuzuia maambukizi mapya ya VVU uongezwe.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
17 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
17 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Nukta TV

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Nukta TV

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Nukta TV