Ahueni, maumivu: Bei ya mchele ikipanda Dodoma

September 7, 2020 1:04 pm · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Bei ya jumla ya zao hilo imepanda kwa Sh55,000 ndani ya kipindi cha wiki moja. 
  • Itakuwa kicheko kwa wafanyabiashara na maumivu kwa wanunuzi. 

Dar es Salaam. Wafanyabiashara wa mchele katika jiji la Dodoma leo watalala na tabasamu baada ya bei ya jumla ya zao hilo kupanda kwa Sh55,000 ndani ya kipindi cha wiki moja. 

Takwimu za mazao makuu ya chakula zilizotolewa leo (September 7, 2020) na Wizara ya Viwanda na Biashara zinaonyesha kuwa bei ya juu ya gunia la kilo 100 la zao hilo linauzwa kwa Sh220,000 katika soko la Majengo jijini humo ikiwa imepanda kutoka Sh165,000 iliyorekodiwa Jumatatu Agosti 31, 2020.

Hiyo ni sawa na kusema wafanyabiashara hao wataweka kibindoni Sh55,000 kwa kila gunia moja la mchele wanalouza leo sokoni. 

Pia takwimu hizo ambazo hutolewa mara tatu kwa wiki, zinaonyesha kuwa bei ya chini ya mchele jijini humo imepanda hadi Sh160,000 kutoka Sh110,000 iliyorekodiwa wiki iliyopita katika soko hilo hilo la Majengo. 

Kwa bei hizo zinazotumika leo, itakuwa ni maumivu kwa wanunuzi na kicheko kwa wafanyabiashara ambao kupanda kwa bei za mazao ndiyo faida kwao. 

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.