Accra kuwa mji mkuu wa dunia wa vitabu mwaka 2023

September 23, 2021 5:33 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Inakuwa jiji la 23 kupata hadhi hiyo tangu kuanzishwa kwa tukio hilo mwaka 2001.
  • Ghana inaamini vitabu vinaweza kuleta mabadiliko ya kitamaduni na utajiri wa nchi hiyo.

Dar es Salaam. Mji mkuu wa Ghana, Accra umetangazwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (Unesco) kuwa mji mkuu wa dunia wa vitabu kwa mwaka 2023.

Accra inakuwa jiji la 23 kupata hadhi hiyo tangu kuanzishwa kwa tukio hilo mwaka 2001. Miji mingine ya Afrika iliyowahi kupata hadhi hiyo ni Port Harcourt nchini Nigeria mwaka 2014 na Conakry Guinea mwaka 2017.

​Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo, Audrey Azoulay amesema kuwa hatua hiyo inazingatia tathmini ya kamati ya ushauri ya miji ya vitabu ya dunia baada ya kupitia andiko la Accra la kupanua wigo wa usomaji vitabu.

Mpango wa Ghana unatambua jinsi vitabu vinavyoweza kuleta mabadiliko ya kitamaduni na utajiri wa nchi hiyo kupitia watoto na vijana na hivyo kujenga kizazi kijacho chenye stadi thabiti.

Unesco imesema watakaojumuishwa kwenye mpango huo ni makundi yaliyo pembezoni yenye kiwango cha juu cha kutokujua kusoma na kuandika wakiwemo wanawake, vijana, wahamiaji, watoto wanaozurura mitaani na watu wenye ulemavu.

Sherehe zitaanza Aprili  23mwaka 2023 ambayo ni siku ya vitabu na hakimiliki duniani.

Mkakati wa utekelezaji unajumuisha kusambaza vitabu vya kusoma ili kujenga tabia ya kusoma vitabu ambapo pia sekta ya uchapishaji vitabu nayo inapatiwa hamasa.

Accra inatumia mbinu mbalimbali za kuhamasisha kusoma kwa kuanzisha pia maktaba tembezi sambamba na kufanyika kwa warsha za kuhamasisha uandishi wa vitabu kwa lugha mbalimbali za Ghana.

Andiko la Ghana kuweza kupata hadhi pia liligusia pia uhuru wa mtu kupata taarifa ikiwa ni kuelekea siku ya uhuru wa vyombo vya Habari mwaka 2023.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
21 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
21 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwanzo mwisho mapokezi ya Rais wa Namibia Netumbo Nandi Ikulu Dar es Salaam

Mwanzo mwisho mapokezi ya Rais wa Namibia Netumbo Nandi Ikulu Dar es Salaam

Nukta TV

Sikia kisa cha bibi wa Mbagala, chanzo Jaji Mkuu Masaju kupanda cheo

Sikia kisa cha bibi wa Mbagala, chanzo Jaji Mkuu Masaju kupanda cheo

Nukta TV

FAHAMU KUHUSU SIKOSELI | Part 1: Ugonjwa wa kurithi, unaotesa maelfu ya watoto Tanzania

FAHAMU KUHUSU SIKOSELI | Part 1: Ugonjwa wa kurithi, unaotesa maelfu ya watoto Tanzania

Nukta TV