Serikali yapendekeza kuondoa VAT nguo za pamba ya Tanzania
Dar es Salaam. Serikali ya Tanzania inapendekeza kusamehe kodi ya ongezeko la thamani (VAT) kwenye nguo na mavazi yanayozalishwa kwa kutumia pamba inayozalishwa ndani ya nchi (locally grown cotton) kwa lengo la kuhamasisha matumizi yake.
Waziri wa Fedha Balozi Khamis Mussa Omar amesema bungeni Dodoma leo kuwa pia wanapendekeza kuongeza ushuru wa forodha kutoka asilimia 25 hadi asilimia 35 au dola za Marekani 0.30 kwa mita ya kitambaa kutegemea kiwango kitakachokuwa kikubwa.
Hatua hizo za Serikali zinatokana na umuhimu wa mchango wa tasnia ya pamba, nguo na mavazi katika uchumi na kulinda viwanda vya ndani.