Tume ya uchunguzi matukio ya Oktoba 29 kuwasilisha ripoti Aprili 23

April 21, 2026 4:42 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni baada ya kuongezewa muda mara mbili.
  • Watanzania 63,603 watoa maoni.

Arusha. Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya kabla na baada ya uchaguzi mkuu, inatarajiwa kukabidhi ripoti yake kwa Rais Samia Suluhu Hassan, Alhamisi ya Aprili 23, 2026 baada ya kuongezewa muda mara mbili.

Ripoti hiyo huenda ikawa miongoni mwa mambo yanayosubiriwa kwa hamu kubwa na Watanzania, baada ya kuongezewa muda mara kadhaa tangu kuundwa kwa tume hiyo miezi mitano iliyopita.

Tume hiyo ilianza rasmi kutekeleza majukumu yake Novemba 20, 2025, mara baada ya kuzinduliwa na Rais Samia na ilitarajiwa kukamilisha kazi zake pamoja na kuwasilisha taarifa ndani ya kipindi cha siku 90, yaani kabla au ifikapo Februari 20, 2026.

Tofauti na matarajio ya wengi tume hiyo ilitangaza kuongezewa muda wa siku 42 na kutakiwa kuwasilisha ripori hiyo kabla au ifikapo Aprili 3, 2026 ahadi ambayo haikutekelezeka.

Aprili 7 mwaka huu tume hiyo ilitangaza kuongezewa tena muda wa siku 21 ikitakiwa kukamilisha kazi hiyo kabla au ifikapo Aprili 24, 2026 suala lilioibua maswali miongoni mwa wananchi na wadau wa masuala ya haki za binadamu nchini.

Kwa mujibu wa Jaji Chande Tume hiyo imepokea ushahidi kutoka kwa Watanzania 63,603 kwa njia mbalimbali. 

Amesema ushahidi huo umepatikana kupitia mahojiano ya ana kwa ana yaliyohusisha watu 1,323, mashahidi wa viapo (affidavit) watu 553, madodoso yenye maswali bila kutaja majina ya wahusika watu 4,891, pamoja na mikutano ya makundi 202.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HOTUBA YA BAJETI OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA)

🔴LIVE: HOTUBA YA BAJETI OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA)

Nukta TV

Yaliyojiri Bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya Vijana ikisomwa kwa mara ya kwanza

Yaliyojiri Bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya Vijana ikisomwa kwa mara ya kwanza

Nukta TV

Maendeleo ya Vijana yaomba kuidhinishiwa Sh35.9 bilioni bajeti 2026/27

Maendeleo ya Vijana yaomba kuidhinishiwa Sh35.9 bilioni bajeti 2026/27

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.