Rais Samia aunda tume ya uchunguzi wa kijinai matukio ya Oktoba 29

May 18, 2026 10:05 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Tume hiyo inaundwa wiki tatu tangu tume ya Jaji Chande iwasilishe ripoti yake kwa Rais Samia.

Arusha. Rais Samia Suluhu Hassan ameunda tume ya uchunguzi wa kijinai ya matukio ya ghasia ya wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 itakayoongozwa na Jaji  Shabani Ally Lila.

Taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi Dk Moses Kusiluka, iliyotolewa leo Mei 18, 2026 imebainisha kuwa uamuzi huo umetokana na mapendekezo ya Tume ya Rais ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani Yaliyotokea Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2025 na kwa kuzingatia mamlaka ya Rais chini ya Sheria ya Tume za Uchunguzi, Sura ya 32.

Tume hiyo inaundwa baada ya takribani wiki tatu tangu tume ya kuchunguza matukio ya vurugu za wakati na baada ya uchaguzi mkuu maarufu kama tume ya Jaji Chande iwasilishe ripoti yake mbele ya Rais Samia ikibainisha mapendekezo yaliyolenga kuponya Taifa baada ya kupitia kipindi hicho cha ghasia.

Hata baada ya kuwasilisha ripoti hiyo iliyochukua siku 153 kukamilika, tume hiyo iliendelea kosolewa vikali na watetezi wa haki za binadamu na vyama vikuu vya upinzani ikiwemo Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Watatu wateuliwa

Mbali na Jaji Shabani, taarifa ya Kusiluka imeeleza kuwa Rais Samia Suluhu Hassan amewateua pia majaji wastaafu watatu wa Mahakama Kuu ya Tanzania ambao ni Gad John Mjemmas, Awadh Mohammed Bawazir na Aishieli Nelson Sumari. 

Aidha, Taarifa hiyo haijabainisha lini wateule hao wataapishwa rasmi kwa ajili ya kuanza kazi.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
9 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
9 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Ulinzi waimarishwa Dar, maduka yachelewa kufunguliwa

Ulinzi waimarishwa Dar, maduka yachelewa kufunguliwa

Nukta TV

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV