HESLB yatangaza majina waliopata mikopo awamu ya kwanza 2025/26

October 24, 2025 3:09 pm · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link
  • 40,952 ni wa shahada ya kwanza na 5,342 wa stashahada ambao wamepangiwa mikopo yenye thamani ya Sh152 bilioni.

Dar es Salaam. Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetoa awamu ya kwanza ya upangaji mikopo na ruzuku kwa jumla ya wanafunzi 135,240 nchini.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, leo Ijumaa, Oktoba 24, 2025, kati ya wanafunzi hao, 40,952 ni wa shahada ya kwanza na 5,342 wa stashahada ambao wamepangiwa mikopo yenye thamani ya Sh152 bilioni.

Aidha, wanafunzi 615 waliopo chini ya mpango wa Samia Scholarship wamepangiwa ruzuku yenye jumla ya Sh3.3 bilioni.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa wanafunzi 88,331 wanaoendelea na masomo wamepangiwa mikopo yenye thamani ya Sh271.2 bilioni baada ya kufaulu mitihani yao ya mwaka uliopita.

Bodi hiyo imebainisha kuwa itaendelea kutoa awamu nyingine za mikopo na ruzuku kadiri itakavyopokea uthibitisho wa udahili kwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza na matokeo ya wanafunzi wanaoendelea.

HESLB pia imewakumbusha waombaji wa mikopo na ruzuku kuendelea kufuatilia taarifa za maombi yao kupitia mfumo wa Student’s Individual Permanent Account (SIPA) wakati taratibu za uchambuzi na upangaji zikiendelea.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
16 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
16 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Nukta TV

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Nukta TV

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Nukta TV