Polisi wazua mkutano wa Chadema na wanahabari Dar es Salaam

January 27, 2025 1:59 pm · Davis Matambo
Share
Tweet
Copy Link
  • Wazingira ofisi ya Chadema wakiwa na silaha na kuzuia watu kuingia ndani wakiwemo watumishi wa Chadema

Dar es Salaam. Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam limezua kufanyika kwa mkutano baina ya waandishi wa habari na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), John Mnyika uliopangwa kufanyika leo Januari 27 kwenye ofisi za makao makuu ya chama hicho Mikocheni, Dar es Salaam.

Nukta habari imefika katika ofisi za hizo na kushuhudia askari polisi wakiwa wenye silaha wakiwa wametanda nje ya geti wakiwaamuru waandishi wote wa habari waliofika kwa ajili ya mkutano huo kuondoka.

Kwa mujibu wa Apolinali Boniface, Msaidizi wa Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya nje wa Chadema, Jeshi la Polisi halijawapa taarifa yoyote ya sababu zilizopelekea kuzuiliwa kufanyika kwa mkutano huo.

“Wamepaki gari nje wanazuia mtu yeyote ambae unakuja ofisini, hata watumishi wa Chadema waliokuja baada ya wao kufika,” amesema Boniface.

Nukta Habari imefanya juhudi za kumtafuta Kamanda wa Polisi Kanda maalum ya Dar es salaam, Jumanne Murilo ili kupata ufafanunuzi wa sababu za kuzuiwa kwa mkutano huo lakini simu yake imepokelewa na msaidizi wake aliyesema Murilo yupo kwenye kikao na atatoa taarifa juu ya zuio hilo.

Baadhi ya vyombo vya habari kikiwepo Jambo TV vimeainisha kuwa, huenda kuzuiliwa huku kunasababishwa na kuwepo kwa mkutano wa Kimataifa wa Nishati ‘Mission 300’ hivyo ungetakiwa kusogezwa mbele baada ya Januari 28 utakapomalizika.

Mkutano huo unahusisha wakuu cha nchi za Afrika na una malengo ya kujadili masuala ya nishati na maendeleo.

https://twitter.com/i/status/1883789755231699118
Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
25 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
25 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa wananchi kupima afya, kuacha uoga

Rais Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa wananchi kupima afya, kuacha uoga

Nukta TV

Uwepo wa vifaa, madaktari uendane na huduma inayotakiwa

Uwepo wa vifaa, madaktari uendane na huduma inayotakiwa

Nukta TV

Rais Samia: Maradhi ya moyo, saratani kwa watoto yaongezeka Tanzania

Rais Samia: Maradhi ya moyo, saratani kwa watoto yaongezeka Tanzania

Nukta TV