Kesi ya Kabendera yaahirishwa kwa saa 24

February 10, 2020 9:05 am · Nuzulack Dausen
Share
Tweet
Copy Link
  • Imeahirishwa hadi kesho Februari 11, 2020 kutokana na kutokamilika upelelezi. 
  • Hii ni mara ya kwanza kesi hii inaahirishwa na kupangiwa terehe ya karibu zaidi kwa siku moja pekee.

Dar es Salaam. Kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili mwandishi wa habari za uchunguzi, Erick Kabendera imeahirishwa hadi kesho kutokana na kutokamilika upelelezi. 

Mashtaka yanayomkabili mwanahabari huyo anayeandikia  vyombo vya habari vya ndani na nje ya nchi ni kuongoza kundi la uhalifu kwa lengo la kupata faida au manufaa mengine, kutokulipa kodi kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ya zaidi ya Sh173.24 milioni na utakatishaji wa fedha kiasi cha  zaidi ya Sh173.24 milioni.

Wakili wa Serikali, Faraji Nguka ameiambia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam leo (Februari 10, 2020) kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika hivyo anaomba ipangiwe tarehe nyingine ya kutajwa.

Kesi hiyo iliyopo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Janeth Mtega ilifikishwa mahakamani leo kwa ajili ya kutajwa.

“Uchunguzi wa kesi hii unaendelea na ikikupendeza Mheshimiwa Hakimu uipangie tarehe nyingine ya kesho,” amesema Nguka.


Soma zaidi: 


Wakili kiongozi wa Kabendera, Jebra Kambole ameiambia mahakama kuwa hawana na kipingamizi juu ya maombi hayo ya wakili wa Serikali.

Mtega ameiahirisha kesi hadi kesho.

Hii ni mara ya kwanza kesi hii inaahirishwa na kupangiwa terehe ya karibu zaidi kwa siku moja pekee.

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW