Mafundi sanifu, michundo kupigwa msasa zaidi

May 24, 2019 3:34 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link

Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili Wahandisi (ERB), Professa Ninatubu Lema, amesema kuwa wasanifu majengo wanahitajika kujituma ili kuanzisha viwanda vidogo vidogo vya kutengeneza bidhaa mbalimbali. Picha|Mtandao.


  • Serikali imesema inaratibu mafunzo ya kuwajengea uwezo ili kuongeza idadi ya wataalam hao.
  • Itawahusisha katika miradi ya ujenzi wa miundombinu ya reli ya kisasa (SGR) na daraja la Selander.
  • Pia kupelekwa nje ya nchi kujifunza ujenzi wa viwanda vidogo vidogo.

Dar es Salaam. Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano imesema itaendelea kuwajengea uwezo na uzoefu mafundi sanifu na mafundi michundo kuwawezesha kutekeleza kazi zao kwa ufanisi na kuziba pengo la wataalam hao katika katika sekta ya ujenzi. 

Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Dk Elius Mwakalinga aliyekuwa akizungumza  jijini Dar es Salaam katika mkutano wa wasanifu majengo na mafundi michundo, amesema kuwa Serikali imejikita katika kuhakikisha sekta ya ujenzi wa miundombinu hasa majengo inafanikiwa kwa kuwa na watalaam wengi wenye weledi.

“Serikali imedhamiria kujenga miundombinu ili kuwezesha ukuaji wa sekta ya Viwanda nchini, hivyo mafundi sanifu wanategemewa sana katika kuwezesha miundombinu hii, ili Tanzania iweze kufikia ndoto ya kuwa kwenye uchumi wa kati kupitia viwanda.

“Katika kutekeleza hilo mwaka wa fedha 2019/2020, Wizara ya Ujenzi imejikita katika ajenda tatu ikiwemo kuwajengea uwezo wasanifu na wahandisi wote nchini,” amesema Dk Mwakalinga.


Soma zaidi:


Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Idara ya Habari Maelezo leo, Serikali itahakikisha watalaam chini ya taaluma ya uhandisi, usanifu majengo, ukadiriaji majenzi wanaongezeka kiidadi na kujengewa ujuzi mahususi ili kuwa na uwezo wa kumudu mahitaji ya nchi.

Katika kufanikisha hilo, kuanzia Julai Mosi mwaka huu, Serikali kwa kushirikiana na bodi mbalimbali za taaluma za kihandisi wataanza kuwaweka wataalam hao katika miradi inayotekelezwa nchini ikiwemo ujenzi wa reli ya kisasa (SGR), ujenzi wa ‘Interchange’ ya Ubungo, ujenzi wa bwawa kubwa la kuzalisha umeme mto Rufiji na ujenzi wa daraja la Selander ili wapate uzoefu.

Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili Wahandisi (ERB), Professa Ninatubu Lema, amesema kuwa wasanifu majengo wanahitajika kujituma ili kuanzisha viwanda vidogo vidogo vya kutengeneza bidhaa mbalimbali.

Amesema wanaangalia namna ya kwenda kujifunza katika nchi za China na India jinsi mafundi wao wanavyohusika katika ujenzi wa viwanda vidogo ili kuwaongezea maarifa wataalam wa Tanzania. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
21 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
21 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
21 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwanzo mwisho mapokezi ya Rais wa Namibia Netumbo Nandi Ikulu Dar es Salaam

Mwanzo mwisho mapokezi ya Rais wa Namibia Netumbo Nandi Ikulu Dar es Salaam

Nukta TV

Sikia kisa cha bibi wa Mbagala, chanzo Jaji Mkuu Masaju kupanda cheo

Sikia kisa cha bibi wa Mbagala, chanzo Jaji Mkuu Masaju kupanda cheo

Nukta TV

FAHAMU KUHUSU SIKOSELI | Part 1: Ugonjwa wa kurithi, unaotesa maelfu ya watoto Tanzania

FAHAMU KUHUSU SIKOSELI | Part 1: Ugonjwa wa kurithi, unaotesa maelfu ya watoto Tanzania

Nukta TV