Benki ya Dunia yatoa Sh1.1 bilioni kuboresha maisha ya Watanzania

September 13, 2019 12:58 pm · TULINAGWE ALSON
Share
Tweet
Copy Link
  • Fedha hizo ni kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa kijamii unaolenga kuboresha maisha ya watu wanaoishi katika kaya maskini wakiwemo wanawake na watoto.
  • Pia utasaidia kuongeza mahudhurio ya wanafunzi katika shule za msingi na sekondari. 

Dar es Salaam. Benki ya Dunia imetoa dola za Marekani milioni 450 sawa na Sh1.1 bilioni kwa Tanzania kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa kijamii unaolenga kuboresha maisha ya watu wanaoishi katika kaya maskini wakiwemo wanawake na watoto.

Mradi huo uliopewa jina la “Second Productive Social Safety Net Project (PSSN II)” utatekelezwa na kusimamiwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf) ambapo unakusudia kuwafikia Watanzania zaidi ya milioni 5 ambao nusu yao watakuwa ni wanawake.  

Fedha hizo zilizotolewa na Benki ya Dunia zitasaidia katika uboreshaji wa matumizi ya chakula na njia za kuishi, kuongeza mahudhurio ya wanafunzi katika shule za msingi; pia upatikanaji wa huduma bora za afya. 

Kwa mujibu wa taarifa ya benki hiyo iliyotolewa jana, mradi huo ni muendelezo wa mradi wa kwanza (PSSN II) ambao ulitekelezwa kati ya mwaka 2009 na 2012 katika Wilaya ya tatu za Tanzania na ambao hadi kufikia 2015 ulifanikiwa kuboresha maisha ya kaya takriban milioni moja.  


Zinazohusiana:


Mkurugenzi Mkaazi wa Benki ya Dunia Tanzania, Bella Bird amesema mradi huo utawasaidia wanufaika katika kudunduliza pesa na kupata mali lakini kuokoa maisha ya watu wengi.

“Mradi umesaidia watu wengi katika kutekeleza shughuli nyingi muhimu zikiwemo kuweka pesa pamoja na kupata mali (Assets) nyingine nyingi, hivyo imesaidia kupata chakula kingi zaidi, elimu bora pamoja na afya bora.

“Bado msaada huu utakuwa wenye manufaa kwa watu wengi katika sekta mbalimbali,” amesema Bird. 

Tofauti na mradi wa kwanza uliowalenga zaidi vijana lakini huu wa pili unakusudia kuwainua wanawake na watoto kiuchumi na kuwaondolea umasikini katika kaya zao.

Mradi huo unaenda sambamba na mikakati ya Serikali ya kuwaondolea Watanzania umaskini kwa kuboresha miundombinu na huduma za jamii

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
16 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
16 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
16 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Magonjwa haya matano yanayoongoza kwa kuua watu duniani

Magonjwa haya matano yanayoongoza kwa kuua watu duniani

Nukta TV

Mambo yakuzingatia kabla ujawasha gari lako asubuhi

Mambo yakuzingatia kabla ujawasha gari lako asubuhi

Nukta TV

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Nukta TV