Vipi, tukuletee Konyagi ama Chibuku?

January 23, 2020 12:45 pm ยท Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam. Ukiachana na bia, vilevi vingine vinavyozalishwa kwa wingi viwandani #Tanzania ni Konyagi na Chibuku. Takwimu rasmi zinaonyesha bia lita 412.6 milioni zilizalishwa mwaka 2018 zikifuatiwa na Konyagi.

Uzalishaji wa bia mwaka huo, kwa mujibu wa Kitabu cha Hali ya Uchumi wa Taifa mwaka 2018, ulikuwa ni mara nane zaidi ya lit azote za Konyagi na Chibuku. Chibuku ni moja vilevi vya kiwandani vyenye bei nafuu nchini wakati Konyagi ikisifika kwa kuwa kilevi imara zaidi.

Ukiachana na bia, ambazo zinatengenezwa na kampuni mbalimbali, iwapo utaangalia takwimu hizo kwa kina mwenendo katika baadhi ya miaka mitano iliyopita, Konyagi na Chibuku ni kama zilikuwa zinachuana katika kiwango cha uzalishaji.

Ikumbukwe kuwa vinywaji vyote hivyo viwili vinatoka katika familia moja ya Kampuni ya Bia Tanzania (TBL).

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW