Wagonjwa wa Corona wafikia watatu Tanzania

March 18, 2020 12:04 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Mgonjwa mmoja amekutwa Zanzibar na mwingine jijini Dar es Salaam na kufanya idadi ya wagonjwa kufikia watatu. 
  • Wagonjwa hao wote ni raia wa kigeni ambao wanaendelea kupata matibabu.

Dar es Salaam. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ametangaza ongezeko la wagonjwa wawili wa virusi vya corona Tanzania ambapo mmoja amekutwa Zanzibar na mwingine jijini Dar es Salaam na kufanya idadi ya wagonjwa kufikia watatu. 

Kisa cha kwanza cha mgonjwa wa Corona nchini kilithibitishwa Machi 16, 2020 ambapo mgonjwa huyo alikuwa mwanamke mwenye umri wa miaka 46 ambaye aliwasili Tanzania jana Jumapili kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) akitokea Ubelgiji.

Majaliwa aliyekuwa akizungumza leo (Machi 18, 2020)  kupitia kituo cha televisheni cha Taifa cha TBC 1, amesema wagonjwa hao wote ni raia wa kigeni ambao wanaendelea kupata matibabu.  

“Tayari wagonjwa wawili wamepatikana wana maambukizi ya virusi vya ugonjwa huo, mgonjwa mmoja anatoka Zanzibar ambaye sampuli zake zimeletwa maabara kuu. Yeye ni Mjerumani wa miaka 24 amepata maambukizi kwahiyo sasa yuko kwenye uangalizi.

“Lakini pia hapa jijini Dar es Salaam tuna Mmarekani mwenye miaka 21 naye pia amegulika kuna na virusi vya Corona,” amesema Majaliwa.

Tanzania inakuwa nchi ya tatu ya Afrika Mashariki baada ya Kenya na Rwanda kuthibitisha kuwa na wagonjwa wa virusi hivyo vinavyosambaa kwa kasi duniani.

Aidha, amesitisha masomo kwa vyuo vikuu na vya kati nchini Tanzania kuanzia leo Machi 18, 2020 na kuwataka wanafunzi waliofunga kutorudi vyuoni.


Zinazohusiana


Hata hivyo, amesema shughuli zingine zikiwemo za masoko, maduka, usafiri zitaendelea kama kawaida na kuwataka Watanzania kuendelea kuchukua tahadhari muhimu ikiwemo kuepuka mikusanyiko isiyo ya lazima, na kunawa mikono.

“Huduma za usafirishaji zitaendelea lakini wasafirishaji waendelee kuwaelimisha abiria na hakuna umuhimu wa kuwajaza na wabaki kwenye viti na tuendelee kutoa huduma wakati wote ili Watanzania waweze kupata huduma zote; usafiri, masoko na upatikanaji wa chakula,” amesema Majaliwa.

Takwimu za Shirika za Afya Ulimwenguni (WHO) za hadi jana (Machi 17, 2020) zinaeleza kuwa watu 179,112 wameambukizwa ugonjwa huo duniani huku waliofariki wakifikia 7,426. 

Tahadhari za kuchukua ni pamoja na kuosha mikono, kutumia tishu wakati wa kukohoa na kutoshika mdomo, pua na macho.

/
No matches found for this filter
30 May, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
30 May, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
30 May, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
AKILI UNDE INAVYOIMARISHA HUDUMA ZA AFYA YA KINYWA NA MENO

AKILI UNDE INAVYOIMARISHA HUDUMA ZA AFYA YA KINYWA NA MENO

Nukta TV

WAFAHAMU 'THE BIG FIVE' WA AFRIKA

WAFAHAMU 'THE BIG FIVE' WA AFRIKA

Nukta TV

HIVI NDIVYO UNAWEZA KUSAFISHA MENO YAKO

HIVI NDIVYO UNAWEZA KUSAFISHA MENO YAKO

Nukta TV