Mkakati wa teknolojia kupambana na Corona wazinduliwa Uswisi

June 2, 2020 7:15 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Mkakati huo wa C-TAP utasaidia upatikanaji wa chanjo, matibabu na teknolojia zingine dhidi ya ugonjwa.
  • Nchi 30 duniani na taasisi za kimataifa likiwemo Shirika Afya Duniani (WHO) wamejiunga katika mkakati huo.

Nchi 30 duniani na taasisi za kimataifa likiwemo Shirika Afya Duniani (WHO) wamejiunga katika mkakati wa kiteknolojia (C-TAP) ili kuharakisha upatikanaji wa chanjo, matibabu na teknolojia zingine dhidi ya ugonjwa wa virusi vya Corona.

C-TAP inalenga kuhakikisha chanjo na matibabu ya Corona yanamfikia kila mtu duniani pasipo kujali hali yake. 

Mkakati huo ulipendekezwa kwa mara ya kwanza mwezi Machi na Rais wa Costa Rica Carlos Alvarado ambaye jana amejiunga na Mkurugenzi mkuu wa WHO Dk Tedros Adhanom Ghebreyesus katika uzinduzi rasmi uliofanyika kwa njia ya video mjini Geneva Uswisi.

Dk Tedros ameyakaribisha makampuni na Serikali ambazo zinatengeneza vifaa tiba ili kuchangia muundo wao katika mkakati huu wa tiba. 

“Huu ni wakati ambapo watu wanatakiwa kuweka vipaumbele. Nyenzo za kuzuia, kubaini na kutibu COVID-19 ni masuala muhimu kwa umma ambayo yanahitaji kupatikana kwa wote,” amesema.

C-TAP inatoa fursa ya sehemu moja ambapo patapatikana ujuzi wa kisayansi, takwimu na hati miliki ambavyo vitatumika sawia na jumuiya ya kimataifa katika mapambano ya Corona.


Soma zaidi: 


Kamishina Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Michelle Bachelet amesema endapo janga la COVID-19  halitodhibitiwa haraka litaendelea kusambaratisha maisha, biashara na chumi na kutuathiri watu wote kwa njia moja au nyingine. 

“Hivyo hebu na tujiunge pamoja kubadilishana takwimu na taarifa, kusongesha mbele uhamishaji wa teknolojia na kupanua wigo wa upatikanaji wa madawa na teknolojia za afya,” amesema Bachelet.

C-TAP inakusudia kuchagiza uvumbuzi wa chanjo, madawa na teknolojia zingine kupitia utafiti ulio wazi wa kisayansi, na kuharakisha uzalishaji kwa kusanya uwezo wa ziada wa wazalishaji.

Hii itasaidia kuhakikisha kuwepo kwa fursa sawa za bidhaa ambazo tayari zipo na mpya za afya za kukabili COVID-19.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV