Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza afariki dunia

June 9, 2020 2:33 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Amefariki dunia baada ya kukumbwa na shambulio la moyo ikiwa imesalia miezi miwili kabla ya kukabidhi madaraka kwa Rais mteule Evariste Ndayishimiye.

Dar es Salaam. Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza amefariki dunia baada ya kukumbwa na shambulio la moyo ikiwa imesalia miezi miwili kabla ya kukabidhi madaraka kwa Rais mteule Evariste Ndayishimiye.

Nkurunziza aliyeiongoza Burundi kwa miaka 15, amefikwa na umauti Jumanne (Juni 9, 2020) katika hospitali ya kumbukumbu ya 50 ya Karusi—Mashariki ya kati ya Burundi–baada ya kulazwa kutokana maradhi ya moyo Juni 8, taarifa ya Serikali iliyochapishwa kwenye mtandao wa Twitter imeeleza.

Kiongozi huyo amefariki ikiwa ni takriban wiki tatu tu baada ya nchi hiyo ya Afrika ya Mashariki kukamilisha uchaguzi mkuu ulioshuhudia jenerali wa zamani wa jeshi Ndeyishimiye akishinda kwa asilimia 68.7 ya kura zote.


Soma zaidi:


Ndayishimiye aliteuliwa na chama tawala nchini humo cha CNDD-FDD kuwania nafasi hiyo iliyokuwa ikiwaniwa na wagombea wengine saba katika uchaguzi uliofanyika Mei 20.

Nkurunziza (55) alikuwa akitarajiwa kukabidhi madaraka hayo kwa kiongozi huyo mpya mwishoni mwa Agosti 2020 baada ya kukamilisha kipindi chake cha uongozi.

Kipindi cha mwisho cha utawala wa Nkurunziza kilitawaliwa na mivutano ya ndani ikiwa ni tofauti na siku za awali alipotwaa madaraka hayo mwaka 2005.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
25 May, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 May, 2026
No active movers today
Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MIKOA 5 YA KIPOLISI INAYOONGOZA KWA MAKOSA BARABARANI

MIKOA 5 YA KIPOLISI INAYOONGOZA KWA MAKOSA BARABARANI

Nukta TV

SERIKALI YAKAMILISHA MAZUNGUMZO MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA

SERIKALI YAKAMILISHA MAZUNGUMZO MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA

Nukta TV

🔴LIVE: KAPINGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA 2026/2027 BUNGENI.

🔴LIVE: KAPINGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA 2026/2027 BUNGENI.

Nukta TV