Maswali magumu mikoa 10 maskini zaidi Tanzania

July 1, 2020 1:22 pm · Nuzulack Dausen
Share
Tweet
Copy Link
  • Rukwa ndiyo unaoongoza kwa kuwa na takriban nusu au asilimia 45 ya watu wake ambao hawawezi kumudu mahitaji ya msingi wakati Dar es Salaam ukiwa na watu wachache wasiokuwa na uwezo huo kwa asilimia nane tu

Dar es Salaam. Licha ya kiwango cha umaskini Tanzania kupungua ndani miaka 10 iliyopita nchini Tanzania, bado kuna mikoa inayokabiliwa na kiwango kikubwa cha umaskini wa mahitaji ya msingi ambacho kimewekwa kuwa ni takriban Sh50, 000 kwa mwezi. 

Ripoti ya Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi 2017/18 iliyotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) katikati ya mwaka jana inabainisha kuwa kiwango cha Watanzania wanaoishi chini ya mstari wa umaskini wa mahitaji ya msingi nchini kimepungua hadi asilimia 26.4 mwaka 2017/18 kutoka asilimia 28.2 mwaka 2011/12.

“Umaskini wa mahitaji ya msingi ulishuka karibu kila maeneo kwa kasi katika maeneo ya vijijini. Ndani ya muongo uliopita, uwiano wa Watanzania ambao wapo katika umaskini wa kutopea na ambao hawawezi kumudu kununua chakula kinachoweza kutimiliza viwango vya kilokalori (Kcal) 2,200 kwa siku ulishuka kutoka asilimia 12 hadi asilimia nane,” inasomeka sehemu ya ripoti hiyo.

Hata hivyo, kuna mikoa ambayo zaidi ya theluthi ya watu wake wanaishi chini ya mstari wa umaskini wa mahitaji ya msingi ambao ni Sh49,320 kwa mwezi kwa mtu mzima kwa mujibu wa utafiti huo wa mwaka 2018. 

Baadhi ya mikoa hiyo ni Rukwa, Simiyu, Lindi, Geita, Mwanza, Tabora, Kigoma, Tabora na Singida. 

Rukwa ndiyo unaoongoza kwa kuwa na takriban nusu au asilimia 45 ya watu wake ambao hawawezi kumudu mahitaji ya msingi wakati Dar es Salaam ukiwa na watu wachache wasiokuwa na uwezo huo kwa asilimia nane tu. 

Takwimu hizo zinaibua maswali lukuki juu ya hali katika mikoa 10 inayoongoza kwa kuwa na viwango vikubwa vya umaskini wa mahitaji ya msingi. Miongoni mwa maswali hayo ni kwanini kuna viwango vikubwa vya umaskini katika mikoa hiyo? Ni mikakati gani inaweza kuikwamua na hali hiyo? 

/
No matches found for this filter
30 May, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
31 May, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
31 May, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
AKILI UNDE INAVYOIMARISHA HUDUMA ZA AFYA YA KINYWA NA MENO

AKILI UNDE INAVYOIMARISHA HUDUMA ZA AFYA YA KINYWA NA MENO

Nukta TV

WAFAHAMU 'THE BIG FIVE' WA AFRIKA

WAFAHAMU 'THE BIG FIVE' WA AFRIKA

Nukta TV

HIVI NDIVYO UNAWEZA KUSAFISHA MENO YAKO

HIVI NDIVYO UNAWEZA KUSAFISHA MENO YAKO

Nukta TV