Rais Magufuli afariki dunia kwa maradhi ya moyo Tanzania

March 17, 2021 8:47 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Alikuwa amelazwa katika hospitali ya Mzena jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.

Dar es Salaam. Makamu wa Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ametangaza kifo cha Rais John Magufuli aliyefariki wa maradhi ya moyo katika hospitali ya Mzena jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu.

Mama Samia amelitangazia taifa kupitia Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) Jumatano ya Machi 17, 2021 kuwa Rais Magufuli alifariki Saa 12 jioni baada ya kulazwa hospitali hapo tangu Machi 14 mwaka huu.  

“Ndugu Watanzania kwa masikitiko makubwa nawajulisha kuwa leo 17 machi 2021 majira ya saa 12 jioni tumempoteza kiongozi wetu shupavu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Magufuli ambaye amefariki kwa maradhi ya moyo katika hospitali ya mzena jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.

“Mheshimiwa Rais Magufuli alilazwa 6 Machi mwaka huu katika taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete  kwa tatizo la moyo la mfumo wa umeme ambalo kitaalumu linajulikana kama  Chronic Atrial Fibrillation ambalo alikuwa nalo kwa miaka 10,” amesema Mama Samia kwa machungu.

Mama Samia amelieleza taifa kuwa baada ya kupatiwa matibabu JKCI, Rais Magufuli aliruhusiwa Machi 7, mwaka na kuendelea na majukumu yake.

“Tarehe 14 Machi 2021 alijisikia vibaya na kukimbizwa hospitali ya Mzena ambapo aliendelea na matibabu chini ya uangalizi wa madaktari na wauguzi wa JKCI hadi umauti ulipomkuta,” ameeleza.

Kiongozi huyo amesema mipango ya mazishi ya kiongozi huyo inafanywa na wananchi watajulishwa.  

“Nchi yetu itakuwa katika kipindi cha maombolezo kwa siku 14 na bendera zitapepea nusu mlingoti,” amesema.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV