Guterres: Muziki wa Jazz ni alama ya uhuru, utu
- Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa(UN) Antonio Guterres amesema muziki huo ni alama ya utu na uhuru wa mwanadamu.
- Unaweza kuvuka mipaka iliyowekwa na umaskini na uonevu.
Dar es Salaam. Licha ya kuwa muziki wa Jazz umekuwa ukitoa burudani kwa watu, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa(UN) Antonio Guterres amesema kuwa mirindimo na miondoko yake inaonyesha utu wa kibinadamu usiyoweza kushindwa na ambao unaweza kuvuka mipaka iliyowekwa na umaskini na uonevu.
Mkazo wake wa kuhusu masuala ya usawa, amesema huwapa wanamuziki uhuru wa ubunifu kama watu binafsi wakati wa kufanya matamasha na maonyesho kama sehemu ya sauti ya jamii.
Guterres ametoa ujumbe katika Siku ya kimataifa ya Jazz iliyoadhimishwa huo jana Aprili 30, 2021 huku akieleza kuwa maadhimisho hayo yamekuwa faraja na furaha sio tu kwa kuenzi muziki huo bali kwa uhuru, utofauti wetu na utu wa binadamu.
“Haya ni maadili ambayo Umoja wa Mataifa unafanya kazi kuyalinda na kuyachagiza duniani kote. Tangu kuzinduliwa kwake muziki wa Jazz umekuwa daraja la kuunganisha wengi na jukumu lake la kihistoria la kupambana na ubaguzi na ubaguzi wa rangi linaendelea kuunganisha tamaduni mbalimbali kote duniani,” amesema Guaterres.
Zinazohusiana:
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu huyo wa UN, siku hiyo, tunakumbushwa jinsi Jazz inavyoweza kutoa tumaini, uponyaji na nguvu tunapofanya kazi ya kuujenga ulimwengu bora na wenye amani.
Kwa muongo mmoja uliopita, shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni (UNESCO), limekuwa likitangaza ujumbe huu wa siku ya Jazz kote duniani.
Guterres amehitimisha ujumbe kwake kwa kusema “katika maadhimisho haya ya miaka kumi, hebu tuungane tena kusherehekea ari na maadili ya jazz.”
Latest