Dhana potofu za kuepukwa baada ya kupata chanjo ya Corona

July 5, 2021 12:25 pm · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni kufikiri kuwa kupata chanjo ndiyo mwisho wa kuchukua tahadhari dhidi ya Corona.
  • Baada ya chanjo endelea kuchukua tahadhari ikiwemo kunawa mikono na kuvaa barakoa.

Dar es Salaam. Baadhi ya watu wanafikiri wakipata chanjo ya Corona hawatakiwi kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa huo.

Wanafikiri ndiyo mwisho wa kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni, kuvaa barakoa na ndiyo mwanzo wa kuanza kukusanyika kama ilivyokuwa miaka mitano iliyopita.

Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), hakuna chanjo ya Corona ambayo imetolewa na kuthibitishwa kufanya kazi kwa asilimia 100 kwa watu waliopata chanjo hiyo.

Ni sawa na kusema haujahakikishiwa kuwa usipochukua tahadhari dhidi ya Corona kisa umepata chanjo, hautaupata ugonjwa huo bali utakuwa katika upande salama zaidi kuliko ambaye hajapata chanjo kabisa. 

Licha ya kupata chanjo dhidi ya Corona, WHO inashauri kuendelea kuchukua tahadhari kwa kufuata kanuni za afya zilizotolewa dhidi ya ugonjwa huo unaoendelea kusumbua watu duniani.

Jifunze zaidi kwa kutazama video hii:

                        

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hesabu ya bosi, bei ya mafuta pasua kichwa madereva wa daladala

Hesabu ya bosi, bei ya mafuta pasua kichwa madereva wa daladala

Nukta TV

Sakata bei ya mafuta kupanda latua BoT, Naibu Gavana atoa ufafanuzi

Sakata bei ya mafuta kupanda latua BoT, Naibu Gavana atoa ufafanuzi

Nukta TV

BoT yabakiza Riba ya Benki Kuu 5.75% kudhibiti mfumuko wa bei

BoT yabakiza Riba ya Benki Kuu 5.75% kudhibiti mfumuko wa bei

Nukta TV