Mambo yatakayosaidia utengemavu wa sekta ya utalii Tanzania
Dar es salaam. Kutokana na athari za ugonjwa wa Corona (Uviko-19) katika sekta ya utalii, mambo matano muhimu yanapaswa kupewa kipaumbele ili kuhakikisha utengemavu wa sekta hiyo.
Mambo hayo ambayo yameainishwa katika Ripoti ya 16 ya hali ya uchumi Tanzania mwaka 2021 ya Benki ya Dunia ni pamoja na kuweka mazingira yenye ufanisi, uhakika na uwazi katika uwekezaji na biashara.Â
Vile vile, kuanzisha mfumo madhubuti wa taarifa utakaosaidia kupata takwimu kutoka kwa watalii na kampuni zinazojihusisha na utalii ili kuwawezesha watunga sera kuboresha sekta hiyo.

Latest