Hatua kwa hatua: Safari ya utoaji chanjo ya Corona Tanzania
- Hadi Septemba 26, 2021 dozi 400,000 zilikuwa zimeshatolewa nchini, ikiwa ni mbili ya tano ya mzigo wote ulioingizwa nchini.
Dar es Salaam. Ikiwa ni takriban miezi miwili tangu kuzinduliwa kwa zoezi la utoaji chanjo ya Uviko-19 nchini, jumla ya watu 400,000 wamekwisha chanja chanjo hiyo ikiwa ni asilimia 37.8 au mbili ya tano ya dozi zote zilizopokelewa Tanzania mwishoni mwa Julai mwaka huu.
Ujio wa chanjo hiyo ulikuja baada ya Serikali ya Tanzania kujiunga na mpango wa ‘Covax facility’ kwa ajili ya kupata chanjo dhidi ya Uviko-19 Juni 15, 2021.
Baada ya kujiunga na mpango huo, Julai 24 Tanzania ilipokea dozi 1,058,400 za Johnson & Johnson kutoka Marekani kupitia mpango wa Covax na kuzinduliwa rasmi siku nne baadaye na Rais Samia Suluhu Hassan.
Licha ya kuanza kampeni rasmi ya utoaji chanjo hiyo Agosti 3 mwaka huu bado kiwango kikubwa cha dozi zilizopokelewa hakijatumika ikiwa ni chini ya nusu ya dozi zote kiasi cha kuifanya Serikali kuanzisha kampeni ya nyumba kwa nyumba kushawishi watu wengi zaidi kuchanja. Kuchanja chanjo ya Uviko-19 ni hiyari nchini Tanzania.

Latest
