Walioondolewa kazini kwa kughushi vyeti kulipwa michango yao kuanzia Novemba

October 26, 2022 10:53 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni baada ya Rais Samia kuridhia.
  • Walioondolewa katika utumishi wa umma Oktoba 2016 hadi Aprili mwaka 2017.
  • Wataanza kulipwa Novemba mosi mwaka huu.

Dar es Salaam. Watumishi wa umma walioondolewa kazini kwa kughushi vyeti wataanza kurejeshewa michango yao waliyochangia kwenye Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kuanzia Novemba Mosi mwaka huu. 

Watumishi hao ni wale walioondolewa katika utumishi wa umma wakati wa zoezi la uhakiki wa vyeti lililoendeshwa katika kipindi cha kuanzia Oktoba 2016 hadi Aprili mwaka 2017.

Uhakiki huo uliowatoa katika mfumo wa utumishi wa umma watumishi wasiopungua 14,516 waliobainika kuwa na vyeti vya kughushi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Profesa Joyce Ndalichako akizungumzia kuhusu uamuzi huo leo Oktoba 26, 2022 amesema Rais Samia Suluhu Hassan ameridhia watumishi hao warejeshewe michango yao waliyochangia wakati wakiwa kwenye utumishi. 

“Kufuatilia maelekezo hayo, mifuko ya Hifadhi ya Jamii PSSSF na NSSF itarejesha michango ya wafanyakazi iliyowasilishwa kwenye mifuko hiyo bila kuhusisha michango ya mwajiri,” amesema Prof Ndalichako. 

Zoezi la kuwarejeshea michango hiyo litaanza kufanyika kuanzia Novemba Mosi mwaka 2022 kwa njia ya benki na siyo pesa taslimu.

Prof Ndalichako amesema mtumishi husika aliyeondolewa kazini atapaswa kwenda kwa aliyekuwa mwajiri wake akiwa na picha mbili za ‘passport size’, nakala ya taarifa za benki (Bank Statement) ya akaunti iliyo hai na nakala ya kitambulisho cha Taifa au mpiga kura au leseni ya udereva.

Pia mtumishi atatakiwa kujaza hati ya ridhaa kwa aliyekuwa mwajiri wake.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
26 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
27 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
27 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Nukta TV

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Nukta TV

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Nukta TV