Tanzania kuwa mwenyeji wa mkutano mkubwa wa Afrika wa chakula na kilimo

March 16, 2023 1:14 pm · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Rais Samia kuzindua maandalizi yake kesho Ikulu.
  • Mkutano huo utajadili suluhu za uhakika na usalama wa chakula Afrika. 
  • Tanzania yapigiwa upatu uwekezaji iliofanya sekta ya kilimo. 

Dar es Salaam. Huenda Afrika likaanza kujitosheleza kwa chakula siku zijazo baada ya wadau wa maendeleo na wataalam wa sekta ya kilimo kukutana Tanzania ili kujadili namna ya kupata suluhu ya uhakika na usalama wa chakula barani humo.

Tanzania inatarajia kuwa mwenyeji wa mkutano mkubwa wa Afrika wa masuala ya chakula na kilimo (AGRF) utakaofanyika Septemba 5 hadi 8, 2023. 

AGRF ni jukwaa kuu la kuendeleza ajenda ya kilimo na mifumo ya chakula ambapo msisitizo utawekwa kwa vijana na wanawake kama msingi wa mfumo endelevu wa chakula barani Afrika. 

Mkutano huo wa kila mwaka utawakutanisha watu zaidi ya 3,000 wakiwemo viongozi, watunga sera, wanasayansi, wakuu wa serikali na taasisi za binafsi, wakulima, na vijana ili kujadili na kutafuta suluhu ya usalama wa chakula barani Afrika na maisha bora kwa wote. 

Maandalizi yaanza

Ijumaa wiki hii (Machi 17), Rais Samia Suluhu Hassan atazindua maandalizi ya mkutano huo Ikulu jijini Dar es Salaam, hii ni kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Zuhura Yunus.

Tanzania imechaguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano huo kutokana na hatua kubwa za kimageuzi ambazo Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan imezichukua tangu alipoingia madarakani miaka miwili iliyopita.

Hatua hizo ni pamoja na kuongeza bajeti ya Wizara ya Kilimo mara nne kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Serikali ya Rais Samia pia imetambuliwa kwa mradi wake wa ubunifu wa Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT), ambao unalenga kuwawezesha vijana, ambao ndiyo nguvu kazi kubwa nchini, kuingia katika sekta ya kilimo.

Serikali yake pia imewekeza katika miundombinu ya umwagiliaji, huduma za ugani, pembejeo na ruzuku ya mbolea na mbegu kwa viwango vya juu ili kuimarisha sekta ya kilimo kwa maendeleo ya nchi. 

Serikali ya Tanzania pia imekuwa ikitekeleza mpango wa kilimo unaojulikana kama Ajenda 10/30 wenye lengo la kufanya kilimo kiwe cha biashara na kikue kwa wastani wa asilimia 10 kwa mwaka ifikapo 2030.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia azindua minara 758, aacha maagizo mazito juu ya mkongo wa taifa

Rais Samia azindua minara 758, aacha maagizo mazito juu ya mkongo wa taifa

Nukta TV

JAJI MKUU: Njia za asili ni mojawapo ya njia halali za utatuzi wa migogoro

JAJI MKUU: Njia za asili ni mojawapo ya njia halali za utatuzi wa migogoro

Nukta TV

Hesabu ya bosi, bei ya mafuta pasua kichwa madereva wa daladala

Hesabu ya bosi, bei ya mafuta pasua kichwa madereva wa daladala

Nukta TV