Kadhaa wahofiwa kupoteza maisha, kujeruhiwa gari ikisombwa na maji Mwanza
Mwanza. Baadhi watu wanahofiwa kupoteza maisha na wengine kujeruhiwa mara baada ya gari ya abiria kampuni ya Batco, linalofanya safari zake kati ya Mwanza na Mahaha wilayani Magu, kudaiwa kusombwa na maji mapema asubuhi wakati dereva akijaribu kuvuka daraja la mto Simiyu.
Afisa Habari Wilaya ya Magu Pachal Mashamba amekiri kutokea kwa ajali hiyo na kwamba taarifa zaidi zitatolewa mara baada ya uongozi kufika eneo la tukio.