Mwendo wa kuperuzi: Watumiaji wa intaneti wazidi kuongezeka Tanzania
- Idadi ya Watanzania wanaotumia intaneti imeongezeka hadi kufikia milioni 29.8 mwaka 2021.
Dar es Salaam. Huenda idadi ya Watanzania wanaonufaika na fursa za mtandaoni imeongezeka, baada ya takwimu mpya za mawasiliano kuonyesha kuwa idadi ya Watanzania wanaotumia intaneti imeongezeka hadi kufikia milioni 29.8 mwaka 2021.Â
Fursa zinazopatikana mtandaoni ni pamoja na biashara, ujuzi na maarifa yanayohitajika kuboresha maisha.Â
Ripoti ya takwimu mpya za robo ya nne ya mwaka 2021 za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) zilizotolewa hivi karibuni, zinaonyesha kuwa watumiaji wa intaneti wameongezeka hadi kufikia milioni 29.8 mwaka jana kutoka milioni 28.5 wa mwaka 2020.Â
Hata hivyo, ripoti hiyo haijaweka wazi ni aina gani ya intaneti inayotumiwa zaidi na Watanzania kama ambavyo imekuwa ikifanyika miaka iliyopita, ambapo intaneti inayohamishika (mobile wireless) ambayo hutumika zaidi na simu za mkononi, tableti na kompyuta mpakato ndiyo imekuwa ikitumiwa zaidi na Watanzania.

Latest