Zingatia haya kabla hujaanza kufanya ‘diet’
- Ni pamoja na kuonana na mtaalamu wa masuala ya lishe ili kufahamu vyakula vipi vitakufaa.
Dar es Salaam. Kupunguza mwili huenda ni sehemu ya ratiba ya baadhi ya watu hasa pale anapoona uzito wa mwili unapita kiwango cha kawaida.
Baadhi huchagua kufanya mazoezi ili kupunguza uzito lakini wapo ambao huchagua njia ya kupunguza kiasi cha chakula wanachokula ili kupunguza kasi ya kuongezeka uzito.
Hata hivyo, katika uchaguzi wa kupunguza chakula, umakini unahitajika kuhakikisha kuwa afya yako inabaki kuwa katika mstari na mwili unapata virutubisho stahiki kulingana na mahitaji yake.
Ufanye nini kuhakikisha unakuwa na “diet” ambayo haiingilii afya yako? Tazama video hii kujifunza;
Latest
