Zimamoto yatangaza nafasi za ajira kwa vijana

February 14, 2025 11:26 am · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Ajira hizo ni kwa ajili ya waombaji wenye elimu ya kidato cha nne, kidato cha sita wenye ujuzi maalum, na wahitimu wa shahada katika taaluma mbalimbali.

Arusha. Jeshi la Zimamoto na Uokoaji limetangaza nafasi za ajira kwa vijana wa Kitanzania wenye sifa stahiki, likiwataka kutuma maombi yao kupitia mfumo wa ajira wa jeshi hilo kabla ya tarehe 28 Februari, 2025.

Kwa mujibu wa tangazo lililotolewa na Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo, John Masunga Februari 13, 2025 nafasi hizo ni kwa ngazi ya Konstebo na zinahusisha waombaji wenye elimu ya kidato cha nne, kidato cha sita wenye ujuzi maalum, na wahitimu wa shahada katika taaluma mbalimbali.

Miongoni mwa vigezo vilivyotajwa kwa waombaji ni kuwa na uraia wa Tanzania kwa kuzaliwa, afya njema kimwili na kiakili, kutokuwa na kumbukumbu za uhalifu, kutokuwa na alama za kuchorwa mwilini (tatoo), na kutowahi kutumia madawa ya kulevya. 

Aidha, waombaji wanapaswa kuwa tayari kuhudhuria mafunzo ya taaluma ya Zimamoto na Uokoaji.

Kwa waombaji wa nafasi za madereva wa magari makubwa, wanapaswa kuwa na leseni ya daraja E huku marubani wa helikopta wakihitajika kuwa na umri wa miaka 18 hadi 35. Kwa upande wa wahitimu wa shahada, nafasi za ajira zinazopatokana ni kwa taaluma kama uhandisi bahari, TEHAMA, sheria, uchumi, na uhandisi wa Ndege.

Maombi yote yanapaswa kufanywa kupitia mfumo wa ajira wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa njia ya mtandao kupitia ajira.zimamoto.go.tz, huku nyaraka muhimu kama barua ya maombi, nakala za vyeti vilivyothibitishwa, cheti cha kuzaliwa, na kitambulisho cha utaifa (NIDA) zikiambatanishwa.

Jeshi hilo limeonya kuwa maombi yatakayowasilishwa kwa barua pepe, posta au kwa mkono hayatapokelewa, huku hatua za kisheria zikitarajiwa kuchukuliwa kwa wale watakaowasilisha nyaraka za kughushi au taarifa za uongo.

Hata hivyo, jeshi hilo halijabainisha idadi ya nafasi za ajira zizlizotolewa kwa ajili ya vijana wakitanzania.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
13 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
13 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV