William Lukuvi afariki dunia

March 25, 2026 10:13 am · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Amefariki dunia katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, Jijini Dodoma alipokuwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa mshtuko wa moyo.

Arusha. Aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) na Mbunge wa Jimbo la Isimani (CCM), William Vangimembe Lukuvi amefariki dunia leo Machi 25, 2026, majira ya saa moja asubuhi kutokana na mshtuko wa moyo.

Rais Samia Suluhu Hassan ametangaza kifo cha mbunge huyo kupitia taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dk Moses Kusiluka iliyotolewa leo Machi 25, 2025 ikifafanua kuwa Lukuvi amefariki dunia katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, Jijini Dodoma alipokuwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa mshtuko wa moyo.

Kufuatia msiba huo, Rais Samia ametoa pole kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, familia, wananchi wa Jimbo la Isimani, ndugu, jamaa, marafiki na Watanzania wote.

Lukuvi (70) amepoteza maisha ikiwa ni takribani miezi minne tangu apewe ridhaa ya kuongoza Jimbo la Isimani lililopo mkoani Iringa, akiteuliwa pia kuiongoza Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu).

Kiongozi huyo ambaye ni miongoni mwa viongozi wakongwe zaidi nchini Tanzania akiwa na zaidi ya miaka 30 Bungeni atakumbukwa kwa utendaji kazi wake na ufanisi katika siasa ulimuwezesha kuwapika wanasiasa wachanga.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Follow Us on TikTok

Subscribe to Our YouTube Channel

Subscribe

Loading videos...

Loading videos...

Loading videos...

Enable Notifications OK No thanks