Vodacom yaibuka na mfumo mpya wa kidigitali

October 2, 2020 12:49 pm · TULINAGWE ALSON
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni mfumo unarahisisha utoaji huduma za kampuni hiyo ya simu ikiwemo M-Pesa.
  • Unaweza kuunganishwa na programu mbalimbali kuwasaidia wananchi kufanya biashara kwa urahisi. 
  • Wabunifu watakiwa kutoa mazao yatakayoboresha zaidi mfumo huo.

Dar Es Salaam. Wateja wa kampuni ya Vodacom Tanzania, sasa wana kila sababu ya kutabasamu baada ya kampuni hiyo kuzindua mfumo wa kidijitali unaorahisisha utoaji wa huduma zake ikiwemo ya M-Pesa. 

Mfumo huo mpya wa kiteknolojia (Application Programing Interface) unajumuisha programu za simu (Apps) za M-Pesa na “My Vodacom App” ambazo zinawawezesha watumiaji wa simu janja kupata huduma kwa urahisi na haraka.

Mfumo huo (Application Programing Interface-API) pia unawezesha uunganishaji wa mifumo ya malipo katika mfumo wa huduma za kifedha wa M-Pesa uwe rahisi, wa haraka na wenye ufanisi zaidi.

Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Hisham Hendi aliyekuwa akizungumza katika uzinduzi wa mfumo huo Oktoba 1, 2020 jijini Dar es Salaam amesema lengo ni kuunga mkono ubunifu wa mifumo ya kidigitali inayorahisisha utoaji huduma na kuwaletea maendeleo wananchi na Taifa.

“Tunaunga mkono ubunifu wa mifumo ya kidigitali itakayo badilisha maisha ya watu, na ndiyo maana sasa tumefungulia API za M-Pesa ili kurahisisha biashara zenu na watengenezaji wa programu kuunganisha mifumo mingine na mfumo wa M-Pesa,” amesema Hendi.

Mfumo huo unaweza kuunganisha huduma zaidi ya moja, jambo linatoa fursa kwa wabunifu kubuni apps zitakazorahisisha utoaji wa huduma hasa za malipo kwa njia ya simu. 


Zinazohusiana:


Mkurugenzi wa Vodacom M-pesa, Epimack Mbeteni amesema API mpya iliyozinduliwa leo inaongeza ufanisi na kurahisisha uunganishaji wa mifumo ya malipo katika mfumo wa huduma za kifedha kwa njia ya simu za mkononi wa M-pesa.

Mbeteni amewataka wabunifu wa programu za simu na kompyuta kubuni programu zitakazofanya kazi pamoja na mfumo wa Vodacom ili kutoa huduma zilizo bora kwa wateja wao.

“Tunatumaini kwamba tutaona mawazo mengi mapya, programu na biashara mbalimbali zikiunganishwa na mfumo wetu mkubwa kwa ajili ya kutoa huduma zilizoboreshwa zaidi kwa wateja.” amesema Mbeteni.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
16 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
16 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Nukta TV

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Nukta TV

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Nukta TV