VIDEO: Majaliwa atua bandarini, atoa maagizo mazito
- Aagiza usimamizi wa mitambo ya mita za upimaji wa mafuta (Flow Meter) ili kudhibiti upotevu wa mapato ya Serikali.
Dar es Salaam. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameiagiza Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) ihakikishe inaendelea kuimarisha usimamizi wa mitambo ya mita za upimaji wa mafuta (Flow Meter) ili kudhibiti upotevu wa mapato ya Serikali.
Pia, Waziri Mkuu amesema Serikali inataka kuona makusanyo yote ya mapato kutoka katika bandari zote nchini yanayokusanywa na TPA yanaingia katika mfuko mkuu wa Serikali na kwamba haitakubali kubaki na mtu yeyote anayejihusisha na upotevu wake.
Waziri Mkuu ametoa maagizo hayo leo (Machi 3, 2021) baada ya kukagua mitambo ya mita ya mafuta Kigamboni na Kurasini ya Oil Jety (KOJ) kwenye Bandari ya Dar es Salaam.
Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema ameridhishwa na utekelezwaji wa maagizo na maelekezo mbalimbali aliyoyatoa katika vipindi tofauti kuanzia mwaka 2016 alipofanya ziara katika eneo la mitambo ya mita ya mafuta (Flow Meter) ya Kigamboni na KOJ.
Latest