VIDEO: Jinsi maziwa ya mama yanavyoimarisha afya ya mtoto
- Humjengea mtoto kinga ya mwili madhubuti.
- Kumnyonyesha mtoto kutamsaidia mama kurejea hali yake ya kawaida baada ya kujifungua kwa haraka zaidi.
- Mama anatakiwa kumnyonyesha mtoto wake walau kwa mwaka mzima na ndani ya miezi sita ya kwanza, mtoto asipatiwe chakula kingine chochote ikiwemo uji na maji.
Dar es Salaam. Ni kawaida na ni jukumu la mama kumnyonyesha mtoto wake lakini kutokana na wingi wa majukumu, baadhi yao hushindwa na kuishia kuwapa watoto wao maziwa ya kopo.Â
Mbali na kumuongezea gharama mzazi, hali hiyo humnyima virutubisho muhimu mtoto ambaye hatumii chakula kingine isipokuwa maziwa kwa kipindi cha miezi sita ya kwanza.
Kwa mujibu wa Dk Joshua Sultan kutoka taasisi ya taasisi ya Nakua na Taifa Langu (NTL) na Mkurugenzi wa Indigo Afya, mama anatakiwa kumnyonyesha mtoto wake walau kwa mwaka mzima.
Zaidi, ndani ya miezi sita ya mwanzo, mtoto anatakiwa kupewa maziwa kama chakula pekee bila kuongeza uji na maji.
Tazama video hii kujua undani wa faida unazoweza kupata wewe na mtoto wako.
               Â