Utalii wa farasi unavyoweza kubadilisha mtazamo wako wa matembezi

June 18, 2020 12:57 pm · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni kati ya utalii utakaokusogeza karibu zaidi na wanyama pori.
  • Utalii huo ni maarufu nyanda za kaskazini mwa Tanzania na ukanda wa pwani.

Dar es Salaam. Utalii ni zaidi  ya kupanda milima, kuogelea na kufurahia wanyama wa mbugani. Endapo umemaliza kupanda milima yote nchini, umekula vyakula vya kila kabila na umevalia mavazi ya asili ya kila aina vipo vingine vya kuangazia.

Endapo umezoea kumtazama tembo akitetemesha ardhi kwa muondoko wake ukiwa ndani ya gari, unaweza pia kufikiria kufanya hivyo ukiwa juu ya mgongo wa farasi.

Kufanya utalii huo ambao unapatikana nchini katika baadhi ya hifadhi, haihitaji uzoefu mkubwa kwani hautokua peke yako na utapata nafasi ya kujifunza.

Kati ya watoa huduma wa utalii huo ni Kaskazi Horse Safaris ambao wanafanya shughuli za utalii huo kaskazini mwa Tanzania ikiwemo katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro.


Zinazohusiana


Wadau wengine wa utalii huo ni Kilimanjaro Tanzanite Safaris ambao pia wanafanya kazi katika mikoa ya Manyara na Arusha.

Kwa mujibu wa huduma kwa wateja wa kampuni hiyo, kufanya utalii huo inakubidi utoboe mfuko kidogo kwani inagharimu Sh207,990 kwa watalii wa ndani na nje ambapo utatalii kwa saa mbili

Unaweza pia kufundishwa jinsi ya kutalii na farasi na “kama wewe ni mzoefu, unaweza kupata muda wa kujumuika na twiga, tembo na swala.”

Sehemu zingine ni pamoja na Zanzibar Horse Club iliyopo visiwani Zanzibar, Makoa Farm iliyopo mkoani Kilimanjaro pamoja na Hifadhi ya Taifa ya Arusha

Unampango gani kitalii mwaka huu? Endelea kusoma habari za nukta kwa kufahamu taarifa juu ya sehemu mbalimbali za kutalii.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
16 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
16 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Nukta TV

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Nukta TV

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Nukta TV