Ujerumani kuanza kutoa chanjo ya Corona kwa kila mtu Juni

May 19, 2021 6:03 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Itaanza kutoa chanjo hiyo kwa kila mtu kuanzia Juni 7 mwaka huu.
  • Imesema inataka kuwakinga zaidi raia wake.
  • Tanzania yashauriwa kuanza kutoa chanjo kwa raia wake.

Wakati Tanzania ikishauriwa kuanza kutoa chanjo ya Corona kwa raia wake, Waziri wa Afya wa Ujerumani Jens Spahn amesema nchi yake itaanza kutoa chanjo hiyo kwa kila mtu kuanzia Juni 7 mwaka huu.

Mei 17, 2021, Kamati maalum ya iliyoundwa na Rais Samia Suluhu kuchunguza hali ya ugonjwa wa Corona nchini wakati ikiwasilisha ripoti yake ilipendekeza kuwa Serikali iruhusu matumizi ya chanjo dhidi ya ugonjwa huo kwa Watanzania kwani ni salama na zimekidhi viwango vya kisayansi.

Waziri Spahn amewaambia waandishi wa habari jana Mei 18 kuwa mfumo wa sasa wa afya nchini Ujerumani hautazingatia kutoa kipaumbele kwa makundi maalum ya watu wakati wa utoaji chanjo kama ilivyokuwa awali.

Waziri huyo amesema kampeni ya chanjo imeshika kasi katika wiki za hivi karibuni na kwamba mwishoni mwa mwezi huu wa Mei, karibu asilimia 40 ya watu nchini Ujerumani watakuwa wamepata chanjo ya kwanza.


Soma zaidi: 


Amesema hadi sasa asilimia 70 ya wale walio juu ya umri wa miaka 60 tayari wamepokea chanjo ya kwanza na karibu robo yao wamekwisha pewa chanjo kamili. 

Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya kimataifa, dozi za chanjo milioni 40 dhidi ya corona zimetolewa na karibu watu milioni 9  wamepewa chanjo kamili, katika nchi hiyo yenye watu milioni 83.

Mpaka sasa kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Ujerumani imeripoti visa zaidi milioni 3.6 vya Corona na  vifo 86,671. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
13 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
13 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV