Trump adai hakuna tatizo Google kushirikiana na China

July 26, 2019 2:18 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Amesema hakuna tishio lolote la usalama kwa kampuni hiyo kushirikiana na nchi ya China. 
  • Amesema kama kuna tatizo watalibaini tu. 

Rais wa Marekani, Donald Trump amesema haoni kama kuna tishio la usalama kwa nchi yake kutokana na mahusiano yaliyopo kati ya kampuni ya teknolijia ya Google na China. 

Trump ametoa kauli hiyo leo (Julai 26, 2019) katika ukurasa wake wa Twitter, ambapo amesema kama kuna tatizo kwa China kushirikiana na Google watabaini.

“Na matumaini kuwa hakuna tatizo,” ameandika Trump.

Siku 10 zilizopita, Rais huyo alisema kuwa wataichunguza kampuni hiyo jinsi inavyoshirikiana na China katika masula mbalimbali ya teknolojia. 

Trump alifikia uamuzi huo baada ya mfuasi wake na mfanyabiashara wa Marekani, Peter Thiel kuyataka mashirika ya ujasusi ya nchi hiyo ya FBI na CIA kuichunguza kampuni hiyo kwa sababu inaweza kuwa inatumiwa na vyombo vya usalama vya China kuihujumu nchi yake. 

Hata hivyo, Msemaji wa Google, Riva Sciuto amekanusha madai hayo na kusema, “kama tulivyosema kabla, hatufanyi kazi na jeshi la China.” 

Wakati Trump akisema uhusiano wa Google na China hauna tatizo, Marekani bado imeiwekea ngumu kampuni ya simu ya Huawei kufanya kazi na makampuni yake kwa madai kuwa imekuwa ikiisaidia China kuingilia shughuli zake. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
25 Aug, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
25 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Elimu ya kodi mwarobaini wa wafanyabiashara kuikwepa TRA, ianzie shuleni

Elimu ya kodi mwarobaini wa wafanyabiashara kuikwepa TRA, ianzie shuleni

Nukta TV

Rais Samia: Serikali chini ya Magufuli haikutaka kuyumbishwa kukamili kwa JNHPP

Rais Samia: Serikali chini ya Magufuli haikutaka kuyumbishwa kukamili kwa JNHPP

Nukta TV

Rais Samia: Umeme wa SGR hautoingiliwa, Dodoma umeme uhakika 24/7

Rais Samia: Umeme wa SGR hautoingiliwa, Dodoma umeme uhakika 24/7

Nukta TV