Teknolojia ya kilimo inayohimili mabadiliko ya tabianchi
February 21, 2022 9:26 am ·
Rodgers Raphael
Dar es Salaam. Licha ya kilimo kuwa sehemu muhimu ya Watanzania kujipatia kipato, mabadiliko ya tabianchi yamekuwa ni changamoto kubwa inayowabili wakulima.
Mvua zisizotabirika au mafuriko ni miongoni mwa majanga ambayo yamekuwa yakihatarisha uhai wa kilimo.
Hata hivyo, zipo teknolojia ambazo zikitumiwa na wakulima zinaweza kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi na hivyo kuwawezesha kunufaika na kilimo.
