Tanzania mguu sawa Sensa ya Watu na Makazi

June 7, 2022 11:37 am · David
Share
Tweet
Copy Link
  • Majaribio kufanyika Agosti 20 na 21 mikoa 18 nchini.
  • Wananchi waendelea kuhamasishwa kushiriki zoezi hilo.
  • Vijiji, mitaa itakayoshiriki yatajwa.

Dar es Salaam. Serikali ya Tanzania imesema kuwa tayari imekamilisha mchakato wa mitaa na vijiji vitakavyoshiriki katika zoezi la Sensa ya Watu na Makazi linalotarajia kufanyika Agosti 23 mwaka huu.

Waziri wa Fedha na Mipango Dk Mwigulu Nchemba aliyekuwa akiwasilisha bajeti ya wizara yake kwa mwaka 2022/23 leo Juni 7, 2022 bungeni jijini Dodoma amesema hadi kufikia Aprili 22 mwaka huu vitongoji vyote 64,318 na mitaa 4,670 Tanzania bara imetengwa kwa ajili ya zoezi hilo.

Kwa upande wa Zanzibar jumla ya maeneo 4,313 ya kuhesabia watu kutoka shehia (Kata) 388 yametengwa sawa na asilimia 100 ya lengo.

“Kazi nyingine zilizokamilika ni kuandaa madodoso ya sensa ya watu na makazi, sensa ya majengo, sensa ya anwani ya makazi, miongozo ya fomu za kudhibiti ubora, kuandaa mfumo wa ufuatiliaji,” amesema waziri huyo.

Zoezi hilo muhimu linalofanyika kila baada ya miaka 10 litatunguliwa na  sensa ya majaribio itakayofanyika Agosti 20-21 katika mikoa 18 ya Tanzania Bara na Zanzibar.

Sambamba na hilo Serikali inaendelea na mchakato wa kununua vifaa vya sensa na kuandaa rasimali watu katika maeneo husika.


Soma zaidi:


Aidha, Waziri Nchemba ameendelea kuwahamasisha wananchi kujitokeza wakati wa sensa kwani jambo hilo lina umuhimu kwa maendeleo ya nchi.

Baadhi ya wabunge wamepongeza serikali kwa kuendelea na maandalizi ya sensa lakini wamehoji uwepo changamoto kwa watakaotumika kufanya kazi ya sensa kwani baadhi ya watu wanaochaguliwa kufanya kazi ya sensa hawana weledi ya kiutumishi.

“Tumeona kwenye postikodi, kule kwetu kuna asilimia imetekelezeka kwa utendaji mzuri , kuna asilimia imefeli……mtu hana weledi wa kiutumishi anapewa kazi kwa kuwa ina posho ataomba,”  amesema Jerry Slaa,Mbunge wa Ukonga

Aidha Mbunge Slaa amependekeza walimu wapewe kipaumbele katika kazi hiyo kwa sababu wana uzoefu katika utumishi.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
8 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
8 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Ulinzi waimarishwa Dar, maduka yachelewa kufunguliwa

Ulinzi waimarishwa Dar, maduka yachelewa kufunguliwa

Nukta TV

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV