Tanzania itakavyonufaika na mahitaji ya kiuchumi ya SADC

July 9, 2019 3:09 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Manufaa hayo yatafikiwa ikiwa itazingatia vipaumbele vya kujenga viwanda na upanuzi wa soko la bidhaa nje ya nchi.
  • Tanzania ikijipanga vizuri kimkakati inaweza kuwa ghala la chakula na soko la jumuiya hiyo.

Dar es Salaam. Katibu Mkuu mstaafu Ofisi ya Waziri Mkuu, Mussa Uledi amesema Tanzania itaendelea kunufaika na fursa za kiuchumi katika Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) ikiwa itazingatia vipaumbele vya kujenga viwanda na upanuzi wa soko la bidhaa nje ya nchi.

Akizungumza leo (Julai 9, 2019) mjini Morogoro wakati akiwasilisha mada katika mafunzo ya Wanahabari kuripoti habari za SADC, Uledi amesema kuwa  Tanzania imenufaika na utekelezaji wa miradi mbalimbali ikiwemo ya miundombinu,  biashara, uwekezaji  na viwanda ya jumuiya hiyo. 

“Mkakati wa maendeleo wa SADC unafafanana kwa kiwango kikubwa na ule wa Tanzania ambao pia unazingatia haja ya utekelezaji wa viwanda na miundombinu hapa nchini hali itakayochangia katika kuimarisha maendeleo na kukuza uchumi na ustawi wa wananchi,” amesema Uledi.

Amesema kuwa vipaumbele vya Tanzania vimejikita katika upanuzi wa mauzo nje na uongezaji wa michepuo yake, lengo likiwa ni kukuza na kuendeleza biashara hali inayowezesha uendelezaji wa viwanda vya kuongeza thamani kwa kutumia malighafi za ndani hususan mazao ya kilimo na madini.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Idara ya Habari-Maelezo, vipaumbele vingine kuwa ni pamoja na  uendelezaji miundombinu kama barabara, reli, usafiri wa anga, uzalishaji na usambazaji huduma za umeme ambayo ni nyenzo muhimu katika kuyaunganisha masoko ya nchi wanachama wa SADC.

Amesema Tanzania ikijipanga vizuri kimkakati inaweza kuwa ghala la chakula kwa kuongeza uzalishaji kuendana na mahitaji katika soko la jumuiya hiyo na hata nje ya jumuiya hiyo.


Soma zaidi:


Hivi karibuni, Rais John Magufuli alifanya ziara katika baadhi ya nchi za SADC ikiwemo Afrika Kusini na Namibia kabla ya kufanyika kwa mkutano wa 39 wa jumuiya hiyo hapa nchini, Agosti mwaka huu.

Tanzania inatarajiwa kuleta msukumo mpya kwa nchi wanachama wa SADC katika utekelezaji wa miradi na programu za maendeleo za jumuiya hiyo kwa kuwa itakuwa na dhamana kubwa ya kukidhi matarajio makubwa ya nchi wanachama wakati wote wa uenyekiti wake.

Kwa upande wake Mkuu wa Operesheni na Mafunzo, Brigedi ya Magharibi ya Jeshi  la Ulinzi la  Wananchi wa Tanzania (JWTZ),  Kanali Wilbert  Ibuge akizungumza katika mafunzo hayo amesema kuwa  Tanzania ni miongoni mwa nchi za mwanzo kabisa barani Afrika zilizotoa mchango mkubwa na kuratibu kuanzishwa kwa mtengamano wa  SADC.

Amesema hali ya amani na usalama imeendelea kuimarika katika nchi za SADC na kutoa fursa ya kukuza uchumi, kuondoa umasikini na kuboresha hali ya maisha ya wananchi.

Msingi wa SADC ni kusimamia malengo yake ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii sambamba na yale ya ulinzi na usalama unaobainishwa katika Ibara ya 2 ya mkataba wa SADC ( Article 2 of SADC Treaty).

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV