Tahadhari! ‘Ivermectin’ sio dawa ya Uviko-19

September 30, 2022 7:51 am · admin
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni dawa ya kutibu minyoo. 
  • Hakuna dawa iliyothibitika kutibu Uviko-19 mpaka sasa.

Dar es salaam. Kumekuwako na uzushi mwingi  na taarifa potofu kuhusiana na dawa zinazoweza kutibu ugonjwa wa Uviko-19 tangu uliporipotiwa kwa mara ya kwanza mwaka 2019 huko Wuhan nchini China na kuenea maeneo tofauti duniani.

Miongoni mwa uzushi huo ni kwamba matumizi ya dawa ya ‘Ivermectin’ yanaweza kumponya mtu aliyeambukizwa Uviko-19, madai ambayo siyo ya kweli kwa mujibu wa  Shirika la Afya la Duniani (WHO).

Huu ndio ukweli

Kwa Mujibu wa WHO mpaka sasa hakuna dawa iliyothibitishwa kuwa na uwezo wa kutibu Uviko-19 hivyo madai ya dawa ya ‘Ivermectin’  kuponya ugonjwa huo si ya kweli.

Dawa ya ‘Ivermectin’ imetambuliwa na WHO kama dawa ya kutibu maradhi ya tumbo yanayosababishwa na minyoo (parasites) kwa binadamu na wanyama lakini si maalumu kwa kutibu Uviko-19.


Zinazohusiana:


Kwa mujibu wa Taasisi ya Chakula na Madawa ya nchini Marekani (FDA) wameeleza kuwa matumizi holela ya dawa hiyo yanaweza kusababisha kupata shinikizo la chini la damu, kifafa, kutapika, mzio au hata kifo.

Taasisi ya FDA pia wameonya juu ya binadamu kutumia dozi za Ivermectin zilizotengenezwa kwa ajili ya wanyama kwani huwa na uwiano mkubwa wa kemikali tofauti na zile za binadamu.

Chukua tahadhari

WHO katika taarifa yake ya mwezi Machi mwaka 2021, imeeleza katika majaribio 16 yaliyofanyika kwa watu 2,407 hayajaonesha ushahidi kuwa dawa hiyo inaweza kutibu Uviko-19.

Wimbi la taarifa potofu kipindi hiki cha janga la Uviko-19 ni kubwa kutokana na watu wengi kuchukua taarifa kutoka kwa vyanzo visivyo vya kuaminika.

WHO imetoa rai kwa watu kufuatilia taarifa za kiafya kutoka kwenye vyanzo vyake vya kuaminika ikiwemo kurasa zake za mitandao ya kijamii.

Follow Us on TikTok

Subscribe to Our YouTube Channel

Subscribe

Loading videos...

Loading videos...

Loading videos...