Si kweli: Wezi waiba basi la polisi mkoani Mbeya

March 17, 2025 4:09 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Jeshi la Polisi Latangaza kuwasaka waliosambaza taarifa hiyo.

Arusha. Ikiwa wewe ni mtumiaji wa mitandao ya kijamii huenda umekutana na taarifa ya wezi kuiba gari la polisi mkoani Mbeya, taarifa hizo sio za kweli.

Taarifa ya Wilbert Siwa, Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Mbeya iliyotolewa leo Machi 17, 2025 imekanusha kutokea kwa tukio hilo  na kuwataka wannchi kuipuuzia

“Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linakanusha taarifa inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii inayosema “WEZI WAIBA BASI LA POLISI MKOANI MBEYA” na kuiomba jamii kupuuza taarifa hiyo kwani hakuna tukio kama hilo mkoani Mbeya.” imesema taarifa ya Siwa.

Habari hiyo iliyokuwa ikisambaa katika mitandao ya kijamii imechota hisia za watumiaji wengi wa mitandao hiyo kutokana na kutumia muundo na rangi zinatumika na chombo cha habari cha Milard Ayo.

Pamoja na hayo, imetumia picha ya gari ya polisi pamoja na nembo ya polisi katika muundo ambao chombo cha milard Ayo hutumia hivyo kuvutia watumiaji wengi wa mitandao hiyo.

Hata hivyo, Jeshi hilo limebainisha kuwa halina basi lenye namba PT 4037 kama zinavyosomeka kwenye picha mnato iliyoambatishwa kwenye taarifa hiyo huku likitangaza kuwasaka walioa taarifa hiyo.

“Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea na uchunguzi wa kuwabaini waliohusika na utoaji wa taarifa hiyo ya uzushi na kuleta taharuki kwa jamii ili hatua stahiki zichukuliwe dhidi yao,” imesema taarifa ya jeshi hilo.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.