Si kweli: Wezi waiba basi la polisi mkoani Mbeya

March 17, 2025 4:09 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Jeshi la Polisi Latangaza kuwasaka waliosambaza taarifa hiyo.

Arusha. Ikiwa wewe ni mtumiaji wa mitandao ya kijamii huenda umekutana na taarifa ya wezi kuiba gari la polisi mkoani Mbeya, taarifa hizo sio za kweli.

Taarifa ya Wilbert Siwa, Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Mbeya iliyotolewa leo Machi 17, 2025 imekanusha kutokea kwa tukio hilo  na kuwataka wannchi kuipuuzia

“Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linakanusha taarifa inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii inayosema “WEZI WAIBA BASI LA POLISI MKOANI MBEYA” na kuiomba jamii kupuuza taarifa hiyo kwani hakuna tukio kama hilo mkoani Mbeya.” imesema taarifa ya Siwa.

Habari hiyo iliyokuwa ikisambaa katika mitandao ya kijamii imechota hisia za watumiaji wengi wa mitandao hiyo kutokana na kutumia muundo na rangi zinatumika na chombo cha habari cha Milard Ayo.

Pamoja na hayo, imetumia picha ya gari ya polisi pamoja na nembo ya polisi katika muundo ambao chombo cha milard Ayo hutumia hivyo kuvutia watumiaji wengi wa mitandao hiyo.

Hata hivyo, Jeshi hilo limebainisha kuwa halina basi lenye namba PT 4037 kama zinavyosomeka kwenye picha mnato iliyoambatishwa kwenye taarifa hiyo huku likitangaza kuwasaka walioa taarifa hiyo.

“Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea na uchunguzi wa kuwabaini waliohusika na utoaji wa taarifa hiyo ya uzushi na kuleta taharuki kwa jamii ili hatua stahiki zichukuliwe dhidi yao,” imesema taarifa ya jeshi hilo.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
7 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
7 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

Nukta TV