SI KWELI: TEC Yatoa Waraka wa Kusomwa kwa Wiki 10 Mfululizo Katika Parokia Zote

May 3, 2025 4:40 pm · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam. Kumekuwa na waraka unaosambaa kwenye mitandao ya kijamii na majukwaa mbalimbali ya kidijitali, ukidaiwa kuwa umetolewa na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC). Waraka huo unatoa agizo kwamba usomwe katika parokia zote, vigango, na jumuiya ndogondogo kwa muda wa wiki 10 mfululizo.

Waraka huo una kichwa cha habari: “WARAKA WA KICHUNGAJI KUSOMA KATIKA PAROKIA ZOTE, VIGANGO, NA JUMUIYA NDOGO NDOGO ZOTE NCHINI TANZANIA KWA WEEK 10 MFULULIZO.”

Taarifa hii imezua taharuki miongoni mwa waumini na wananchi kwa ujumla, ikiwafanya wengine kuhoji msimamo wa Kanisa Katoliki kuhusu masuala ya kijamii na kisiasa nchini.

UKWELI: Waraka huo ni feki, TEC yakanusha vikali

Nukta Fakti, kupitia uchunguzi wake, imebaini kuwa waraka huo ni wa kughushi na haujatolewa rasmi na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC).

Kupitia tamko lao rasmi, TEC imekanusha vikali kuwepo kwa waraka huo na imetoa rai kwa waamini pamoja na Watanzania wote kupuuza taarifa hizo zisizo za kweli.

Katika taarifa hiyo, TEC imesema: “Tunapenda kuwatangazia waamini na Watanzania wote kwa ujumla, kupuuza kabisa waraka huo ambao haukutolewa na Baraza la Maaskofu, na usio na maslahi yoyote kwa nchi yetu.”

Aidha, uchunguzi umebaini kuwa aina ya mwandiko (font) uliotumika katika waraka huo si ile inayotumika katika nyaraka rasmi za TEC, jambo linaloendelea kuthibitisha kuwa waraka huo umetengenezwa na watu wasiokuwa na mamlaka wala uhusiano wowote rasmi na baraza hilo.

TEC pia imetoa wito kwa waamini na watu wote wenye mapenzi mema kutojihusisha na taarifa au vitendo vyovyote vinavyoweza kuhatarisha amani, mshikamano na upendo miongoni mwa Watanzania.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
24 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
25 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Nukta TV

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Nukta TV

Kozi nzuri za kusoma chuo kikuu Tanzania

Kozi nzuri za kusoma chuo kikuu Tanzania

Nukta TV