SI KWELI: Rais Samia atuma ujumbe wa kutatanisha kupitia ukurasa wake wa X

July 14, 2025 4:30 pm · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam. Katika siku za hivi karibuni, kumesambaa chapisho kwenye mitandao ya kijamii likiwa katika mfumo wa picha ya skrini (screenshot) inayodai kuonesha ujumbe uliotumwa kupitia akaunti rasmi ya Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kwenye mtandao wa X (zamani Twitter).

Chapisho hilo lina maneno ya kutatanisha yanayomhusisha moja kwa moja Rais, likieleza: “Hata ukipiga kelele vip Lissu hawezi kutoka jela na simwachii ng’oo mpaka uchaguzi upite na hakuna kenge yoyote wala hata Mahakama haina uwezo wa kumuachia mpaka mimi Amiri Jeshi Mkuu niamue.”

Mbali na kusambazwa kwenye X, ujumbe huo pia umeonekana kwenye ukurasa wa Facebook unaojiita “ITV Tanzania Breaking News”, ambao si ukurasa rasmi wa kituo cha habari cha ITV.

Taarifa hiyo imezua mijadala mikubwa na taharuki miongoni mwa wananchi, huku wengi wakibaki na sintofahamu kuhusu ukweli na uhalali wa chapisho hilo.

UKWELI: Chapisho hilo ni feki – Halijatolewa na Rais Samia

Uchunguzi uliofanywa na Nukta Fakti umebaini kwamba chapisho hilo ni la kughushi. Hakuna ushahidi kuwa limetumwa na Rais Samia, na halipo kwenye ukurasa wake rasmi wa mtandao wa X.

Aidha, aina ya mwandiko (font) uliotumika kwenye chapisho hilo haulingani na ule unaotumika katika machapisho rasmi ya Rais au ya taasisi za Serikali. Hii ni dalili ya wazi kuwa ujumbe huo umetengenezwa kwa nia ya kupotosha umma au kueneza propaganda zenye lengo la kuchafua jina la uongozi.

Zaidi ya hapo, ITV haina ukurasa wa Facebook unaoitwa “ITV Tanzania Breaking News”. Ukurasa rasmi wa kituo hicho unajulikana kama “ITV Tanzania”. Kutumia jina linalofanana ni njia nyingine ya kupotosha wananchi kwa makusudi.

Katika vipindi vya siasa na kuelekea uchaguzi mkuu, taarifa za kughushi zinazotumia majina ya viongozi wakuu huwa nyingi na huenea kwa kasi. Taarifa hizi zinalenga kupotosha umma, kuchochea hisia, au kuvuruga amani ya nchi.

Tunatoa wito kwa wananchi wote watumie vyanzo rasmi kama ukurasa wa X wa Rais Samia, tovuti ya Ikulu, na vyombo vya habari vilivyosajiliwa. Wafanye uhakiki wa taarifa kwa kutumia majukwaa ya uhakiki kama Nukta Fakti. Tuwe makini na tuwe walinzi wa amani kwa kuchuja taarifa kabla ya kuzisambaza.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
14 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
14 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
14 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV