Si kweli: Maria Sarungi amshinikiza Heche kusaini kanuni za maadili za Uchaguzi  

July 25, 2025 11:55 am · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link
  • Machapisho yanayosambaa hayajachapishwa na vyombo vya habari vya Mwananchi, Jambo Tv na The Chanzo na hayapo kwenye akaunti rasmi ya vyombo hivyo vya habari.
  • Boni Yai hajachapisha madai hayo kwenye akaunti yake rasmi ya Mtandao wa X.

Dar es Salaam. Huenda wewe ni miongoni mwa watu waliokutana na taarifa zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii, hususan mtandao wa Facebook zikidai kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kanda ya Pwani, Boniface Jacob maarufu kama Boni Yai amemtuhumu mwanaharakati Maria Sarungi kumshinikiza Makamu Mwenyekiti wa chama hicho John Heche kusaini kanuni za maadili za Uchaguzi. Uchunguzi uliofanywa na Nukta Fakti umebaini kuwa habari hiyo si ya kweli.

Taarifa hii ya upotoshaji inayosambazwa kama chapisho kutoka akaunti rasmi ya mtandao wa X (zamani Twitter) ya Boniface Jacob maarufu kama Boni Yai linalosomeka “Maria Sarungi ndiye aliyewasiliana na Makamu Heche na kusisitiza tusisaini kanuni za maadili za Uchaguzi. Hakukuwa na utaratibu wa kiofisi uliofuatwa, leo tunasema ukweli haki za wanachama wa CHADEMA zimeporwa na wachache wasiothamini misingi ya demokrasia”.

Chapisho hili ni feki, halijachapishwa kwenye akaunti ya mtandao wa X ya Boni Yai, na aina ya mwandiko unaoonekana kwenye chapisho hilo si mwandiko rasmi unaotumika katika machapisho ya mtandao wa huo.

Katika hatua nyingine machapisho ya kughushi yenye mfanano na chapa za vyombo mbalimbali vya habari vinavyoaminika nchini ikiwemo Mwananchi, Jambo TV na The Chanzo yalionekana yakisambaa mtandaoni yakiripoti taarifa hiyo potoshi kwa vichwa mbalimbali vya habari.

Ukweli ni huu

Uchunguzi uliofanywa na Nukta Fakti umebainisha kuwa taarifa hiyo si ya kweli, kwani machapisho yote yenye mfanano wa vyombo vya habari vya Mwananchi, Jambo Tv na The Chanzo hayakuchapishwa kwenye akaunti rasmi za vyombo hivyo.

Aidha aina ya miandiko (fonts) zilizotumika sio zinazotumiaka katika machapisho rasmi ya vyombo tajwa vya habari.

Pia, chapisho linalosambaa kama chapisho kutoka akaunti rasmi ya Mtandao wa X wa Boni yai, si chapisho halali kwani halijachapishwa kwenye akaunti ya mtandao wa X ya Boni Yai, na aina ya mwandiko unaoonekana kwenye chapisho hilo si mwandiko rasmi unaotumika katika machapisho ya mtandao wa huo.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
14 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
14 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
14 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV