SI KWELI: Freeman Mbowe afukuzwa Chadema

July 22, 2025 5:20 pm · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam. Taarifa za kupotosha zinazosamba kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii kama Facebook, Instagram, na YouTube, ikidai kwamba Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amefukuzwa uanachama na uongozi wa chama hicho.

Baadhi ya machapisho hayo yameonekana yakiwa na vichwa vya habari kama:
“Mbowe Afukuzwa Chadema”, bila kuambatanishwa na ushahidi wowote au chanzo halali kutoka ndani ya chama.

Mfano, katika moja ya machapisho yanayosambaa kupitia mtandao wa Facebook, kuna barua iliyowekwa ambayo inadaiwa kutolewa na Chadema. Sehemu ya maneno ya awali katika barua hiyo inadai

“Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimetangaza rasmi kumfutia uanachama Bwana Freeman Mbowe.”

Ukweli ni huu

Uchunguzi uliofanywa na Nukta Fakti umebaini kuwa hakuna taarifa yoyote rasmi kutoka CHADEMA inayothibitisha kufukuzwa kwa Freeman Mbowe kutoka chama hicho.

Aidha, Nukta Fakti imepitia mitandao rasmi ya chama hicho, ikiwemo tovuti na kurasa zake za kijamii, na hakuna chapisho lolote la barua au taarifa kwa umma inayohusiana na madai hayo. Barua iliyosambazwa kwenye mtandao wa Facebook pia imebainika kuwa ni ya kughushi, kwa sababu.

Haipo kwenye kurasa rasmi za Chadema. Haitumii muundo na mwandiko wa barua rasmi za chama hicho. Imesambazwa na akaunti zisizo na uhusiano wowote rasmi na chama.

Zaidi ya hayo, baadhi ya machapisho ya video na picha yanayodaiwa kutoka kwa vyombo vya habari kama ITV hayapo kwenye kurasa rasmi za taasisi hizo, jambo linalothibitisha kuwa taarifa hizo ni za uongo na zenye lengo la kupotosha umma.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
WAMESANUKA, mbinu mpya ya usafirishaji wa dawa za kulevya yafichuliwa

WAMESANUKA, mbinu mpya ya usafirishaji wa dawa za kulevya yafichuliwa

Nukta TV

CCM yatoa ratiba maombi ya kumrithi Lukuvi, Israel, Lebanon wakisitisha mapigano

CCM yatoa ratiba maombi ya kumrithi Lukuvi, Israel, Lebanon wakisitisha mapigano

Nukta TV

Ridhiwani: Serikali inalenga kuacha tabasamu kwa watumishi wa Umma

Ridhiwani: Serikali inalenga kuacha tabasamu kwa watumishi wa Umma

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.