Shilingi yapata nafuu dhidi ya Euro na Pauni, Agosti 31, 2026
- Wanunuaji wa sarafu hizo watanunua kwa bei nafuu kulinganisha wiki iliyopita, kadhalika wauzaji watapata faida zaidi.
Dar es Salaam. Viwango vya kubadilisha fedha katika benki za CRDB na NMB vimeonesha mabadiliko madogo mwanzoni mwa wiki hii, huku baadhi ya sarafu za kigeni zikipanda na nyingine kushuka ikilinganishwa na viwango vilivyokuwa vikitumika Ijumaa, Agosti 28, 2026.
Kwa mujibu wa viwango vya kubadilisha fedha, leo Jumatatu, Agosti 31, 2026, Dola ya Marekani (USD) imeendelea kuwa katika viwango vilevile katika benki zote mbili, huku CRDB ikiendelea kununua dola moja kwa Sh2,605 na kuuza kwa Sh2,685. NMB nayo imeendelea kununua kwa Sh2,600 na kuuza kwa Sh2,680.
Hata hivyo, katika benki ya CRDB, Euro imeongezeka kidogo upande wa ununuzi kutoka Sh2,931.49 Ijumaa hadi Sh2,931.56 Jumatatu, huku bei ya uuzaji ikibaki Sh3,231.56.

Katika benki ya NMB, mabadiliko makubwa zaidi yameonekana kwenye Euro na Pauni.
Euro imeshuka kutoka Sh2,938 Ijumaa hadi Sh2,934 Jumatatu kwa upande wa ununuzi, huku kiwango cha uuzaji kikishuka kutoka Sh3,212 hadi Sh3,208.
Pauni ya Uingereza (GBP) imepanda kutoka Sh3,443.68 hadi Sh3,444.12 kwa ununuzi, huku upande wa uuzaji ukiongezeka kutoka Sh3,743.68 hadi Sh3,744.12.
Kwa upande wa NMB, Pauni ya Uingereza imeshuka kutoka Sh3,397 hadi Sh3,392 kwa ununuzi, huku kiwango cha uuzaji kikishuka kutoka Sh3,744 hadi Sh3,738.
Kwa upande wa sarafu za kikanda, Shilingi ya Kenya imeongezeka kwa senti moja, kutoka Sh16.95 hadi Sh16.96 kwa ununuzi na kutoka Sh23.95 hadi Sh23.96 kwa uuzaji.