Sh500 milioni kuhamasisha nishati safi ya kupikia vijijini

June 1, 2022 4:50 pm · admin
Share
Tweet
Copy Link
  • Zitasaidia kufanya kampeni kubwa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.
  • Pia Kufanyia tafiti ili kubaini nishati bora ya kupikia.

Serikali ya Tanzania imesema katika mwaka ujao wa fedha 2022/23 itatumia Sh500 milioni kwa ajili ya utekelezaji wa mipango mkakati na miradi ya matumizi ya nishati safi na salama ya kupikia hasa maeneo ya vijijini.

Waziri wa Nishati January Makamba akiwasilisha hotuba ya bajeti ya Wizara ya Nishati ya mwaka wa fedha 2022/23 bungeni jijini Dodoma leo (Juni, 1, 2022) amesema karibu asilimia 89 ya kaya zote nchini zinatumia kuni na mkaa kama chanzo kikuu cha nishati ya kupikia hivyo kusababisha uharibifu wa mazingira pamoja changamoto za kiafya.

“Tumetenga Sh500 milioni ili kufanya kampeni kubwa ya kuhamasisha matumizi bora ya nishati ya kupikia pamoja na tafiti za kubaini nishati bora ya kupikia, mifumo sahihi na vivutio vya kusambaza nishati safi ya kupikia katika maeneo ya vijijini,” Waziri Makamba ameliambia Bunge.

Katika mwaka wa fedha ujao utakaoanza Julai, 1, 2022, wizara hiyo imeomba kiasi cha Sh2.9 trilioni ili kutekeleza majukumu yake na miradi mbalimbali ya maendeleo nchini.

Aidha wizara hiyo imesema katika mwaka ujao wa fedha wizara itaongozwa na vipaombele takribani 12 ikiwemo kukamilisha mazungumzo ya mradi wa kusindika na kuchakata gesi  asilia (LNG) mkoani Lindi pamoja kutekeleza miradi ya kupeleka nishati vijijini.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV