Serikali ya Tanzania yawahakikishia wakulima soko la mazao

July 14, 2020 1:28 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Gerald Kusaya akiwa anakagua mfuko unaotumika kuhifadhia mpunga katika kituo cha manunuzi Uturo wilaya ya Mbarali leo. Picha| Wizara ya Kilimo.


  •  Imewahakikishia wakulima kuwa itaendelea kununua mazao yao kwa ajili ya kuongeza hifadhi ya chakula nchini.
  • Wakala wa Hifadhi ya Taifa ya Chakula (NFRA) kununua na kuhifadhi mazao hayo.

Dar es Salaam. Serikali imewahakikishia wakulima kuwa itaendelea kununua mazao yao kwa ajili ya kuongeza hifadhi ya kutosha na uhakika na usalama wa chakula nchini Tanzania

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Gerald Kusaya amesema hayo wakati alipotembelea kituo cha ununuzi wa zao la mpunga katika kijiji cha Uturo wilayani Mbarali unaofanywa na Wakala wa Hifadhi ya Taifa ya Chakula (NFRA) kanda ya Makambako. 

“Serikali kupitia wizara ya Kilimo itaendelea kununua mazao ya wakulima hususan mahindi na mpunga kwa wingi hivyo wakulima msidanganywe kuwa muda umebaki mfupi wa kupeleka mazao yenu NFRA. Leteni hapa mpunga wenu tutaununua wote” amesema Kusaya.

Amesema wizara imejipanga kuona nchi inaendelea kuwa na usalama wa chakula ndiyo maana anapita mikoani kujionea hali ya uzalishaji wa mazao mbalimbali.  


Zinahusiana: 


Kwa mujibu wa Kaimu Meneja wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Makambako Frank Felix amesema tayari wakala umeshanunua tani 1,700 za mpunga kati ya malengo ya tani 5,000 na mahindi tani 2,933.174 kati 25,000 msimu huu. 

Ununuzi huo wa mazao unaofanywa na NFRA utaongeza ushindani wa bei kwa wanunuzi na hivyo kuwafaidisha zaidi wakulima ambao wamewekeza kwenye kilimo. 

Katika hatua nyingine, Kusaya ametembelea  Chuo cha mafunzo ya Kilimo na Mifugo  ( MAMRE) cha Wanging’ombe mkoani Njombe  na kutoa agizo kuwa wanafunzi wanaoshindwa kulipa ada ya mafunzo wasifukuze badala yake utafutwe utaratibu rafiki.

Kusaya alitoa agizo hilo kufuatia malalamiko ya wanafunzi kusema baadhi yao wameshindwa kuendelea na masomo baada ya kushindwa kulipa ada na michango mingine.

 “Vyuo vyote 29 ( 14 vya serikali na 15 vya binafsi) ni vyangu kwani vinalenga kuzalisha maafisa ugani watakaokwenda kuhudumia wakulima nchini. Nitaendelela kuvisaidia bila kuangalia nani  anakimiliki muhimu vitoe mafunzo bora kwa wanafunzi wa kitanzania” amesema Kusaya.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV