Serikali ya Tanzania kumuenzi bilionea Mufuruki kivitendo

December 11, 2019 12:31 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Yasema itasikiliza maoni ya sekta binafsi yanayolenga kuboresha mazingira ya biashara.
  • Yasema inatambua mchango wake alioutoa katika kutengeneza ajira kwa Watanzania na kukuza uchumi.
  • Alifariki jumamosi nchini Afrika Kusini akiwa na umri wa miaka 60.

Dar es Salaam. Serikali ya Tanzania imeahidi  kuendelea kumuenzi  mfanyabiashara maarufu nchini, Ali Mufuruki kwa kusikiliza maoni ya sekta binafsi yanayolenga kuboresha mazingira ya uwekezaji na biashara nchini. 

Mufuruki ambaye pia ni muhisani na kocha wa masuala ya uongozi, alifariki dunia siku ya Jumamosi (Desemba 7), nchini Afrika Kusini alikokuwa akipatiwa matibabu.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji, Angela Kairuki aliyekuwa akizungumza wakati wa kuaga mwili wa mfabiashara huyo katika ukumbi wa kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC), leo (Desemba 10, 2019) jijini Dar es Salaam, amesema Serikali itamuenzi mfabiashara huyo aliyekuwa nguzo ya sekta binafsi kwa mawazo na vitendo. 

“Serikali tutaendelea kumuenzi Mafuruki kwa maneno na vitendo hasa kusikiliza maoni kutoka sekta binafsi ili kuboresha mazingira ya kufanya biashara hapa nchini,” amesema Kairuki.


Zinazohusiana:


Waziri huyo amesema Serikali inatambua mchango wake alioutoa katika kutengeneza ajira kwa Watanzania na kukuza uchumi kupitia miradi na makampuni aliyokuwa akimiliki. 

Mufuruki alikuwa anamiliki kampuni ya teknolojia ya Infotech Investment Group Limited na maduka ya Woolworth. Pia alikuwa muasisi wa Jukwaa la Maofisa Watendaji Wakuu (CEO Roundtable).

Mwenyekiti wa CEO Roundtable, Sanjay Roughani akithibitisha kifo cha mfanyabiashara huyo Desemba 8, 2019, alisema kuwa Mufuruki alianza kuugua akiwa Dar es Salaam na akapelekwa katika hospitali ya Agha Khan na kisha akapelekwa Afrika Kusini. 

Mfanyabiashara huyo aliyekuwa na miaka 60 aliwahi kuwa mwenyekiti wa bodi ya kampuni ya mawasiliano ya simu ya Vodacom Tanzania na Wananchi Group Holdings.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
13 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
13 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
13 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV