Serikali kutatua migogoro ya ardhi inayomilikiwa na madhehebu ya dini

May 17, 2021 6:26 am · Mariam John
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni maeneo yanayomilikiwa na madhehebu yaliyovamiwa na watu.
  • Serikali yasema itaingilia kati.ili kutafuta muafaka.

Mwanza. Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango ameahidi kutatua migogoro mbalimbali ya ardhi inayohusisha maeneo yanayomilikiwa na madhehebu ya dini yakiwemo makanisa yaliyovamiwa na watu. 

 Dk Mpango amaliyekuwa akizungumza Mei 16, 2021 jijini Mwanza katika ibada maalum ya kumsimika Askofu wa  Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Victoria Nyanza, Zephania Ntuza amesema atamtuma Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi kushughulikia suala hilo.

Dk Mpango amesema amesikia suala hilo na kwamba kanisa la Anglikana liandike barua rasmi ili kutafuta ufumbuzi kwa taasisi za dini kuvamiwa.

”Hili suala nimesikia na naomba kama kanisa mlilete kwa maandishi ili tuweze kulishughulikia na kulipatia ufumbuzi,” amesema

Kuhusu migogoro katika makanisa mbalimbali hapa nchini, Dk Mpango ameeleza kuwa suala hilo linawakatisha tamaa waumini na kuwarudisha nyuma kiroho na kuhatarisha amani ya nchi.

Kwa mujibu wa Dk Mpango, Serikali inapenda kuona taasisi za dini zinaongozwa kwa kufuata taratibu na kanuni walizojiwekea ili kuepuka migogoro mbalimbali.

“Tumechoka  kusikia migogoro hiyo ambayo  inakatisha tamaa na kurudisha nyuma waumini kiimani, kuwagawa na kushindwa kutekeleza mambo ya kuwajenga kiroho,” amesema Dk Mpango.


Zinazohusiana: 


Awali  Askofu mpya wa kanisa hilo Dayosisi ya Victoria ya Nyanza, aliomba Serikali kusaidia kurejesha  maeneo ya kanisa yaliyovamiwa  katika sehemu mbalimbali nchini.

”Niombe kwa ruhusa yako Mheshimiwa Makamu wa Rais,  Serikali itusaidie ili kurejesha maeneo yetu yaliyovamiwa na ikikupendeza tutayaleta haya kwako kwa  maandishi,” amesema Askofu huyo.

Sherehe hizo za kumsimika askofu huyo zilifanyika katika kanisa la Nicolaus Dayosisi ya Victoria ya Nyanza na kuhudhuriwa na waumini, maaskofu na viongozi wa Serikali kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV